• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Majaliwa aweka jiwe la msingi ofisi ya DC Butiama

Posted on: February 28th, 2024

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa leo ameweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama iliyopo katika Kijiji cha Butiama kwenye eneo lenye ofisi za Serikali.

Akizungumza baada ya kuweka jiwe la msingi, Mhe. Majaliwa amepongeza mradi huo na kuahidi kuwa Serikali itaendelea kuleta fedha katika Wilaya ya Butiama kwa sababu ni wilaya mpya na nyumbani kwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Mhe. Majaliwa ameitaka TBA kukamilisha mradi huo kwa haraka ili kuboresha mazingira ya ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama na pia aweze kuhamia katika eneo hilo lenye ofisi nyingine zote za Serikali.  

Wakati huo huo, Mhe. Waziri Mkuu amempongeza Mbunge wa Jimbo la Butiama na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Jumanne Sagini kwa kazi nzuri anayoendelea kuifanya katika jimbo hilo.

Akizungumza wakati wa kuwasalimia wananchi wa Wilaya ya Butiama Mhe. Waziri Mkuu amewashukuru wananchi na viongozi wa Wilaya ya Butiama kwa mapokezi mazuri.

Akitoa taarifa za mradi huo, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Miundombinu Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhandisi Richard Moshi ameelza kuwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara ilitenga fedha kwa ajili ya mradi huo kuanzia mwaka wa fedha 2021/2022 na huendelea kutenga fedha kila mwaka kwa ajili ya ujenzi huo.

Eng. Moshi ameeleza kuwa mradi huo umeanza kutekelezwa tarehe 5 Agosti, 2022 na Mkandarasi wa mradi huo ni Wakala ya Majengo (TBA) kwa gharama ya shilingi 2,041,935,338.32 na muda wa mradi ulikuwa ni miezi 12 hata hivyo muda wa utekelezaji wa mradi huo uliongezwa.

Utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 60 na mpaka wakati huu mkandarasi ameshalipwa shilingi 843,394,728.35 ikiwa ni malipo ya awali na hati za malipo ya pili na ya tatu huku hati ya nne ikiwa imetumwa Hazina kwa ajili ya malipo.

Mhandisi Moshi ameeleza kuwa mradi huo una changamoto ya kasi ndogo ya mkandarasi katika utekelezaji wa mradi inayosababishwa na uwezo mdogo wa kifedha wa mkandarasi hivyo kushindwa kufuata mpangokazi uliowekwa.  

Kwa upande wake, Mhe. Sagini amesema yapo mambo mengi yamefanyika katika Wilaya ya Butiama katika miradi ya maendeleo katika sekta za afya, elimu, Chuo Kikuu cha Butiama na Chuo cha VETA kilichojengwa katika jimbo la Butiama.  

Mhe. Sagini amesema ukarabati wa majengo ya awali ya Chuo kikuu cha Mwalimu Julius K. Nyerere Butiama ukarabati umekamilika, wanafunzi wameanza masomo kwa mwaka huu wa masomo na serikali kupitia mradi wa maendeleo ya Vyuo Vikuu unaofadhiliwa na benki ya Dunia imetoa zaidi ya bilioni 100 na kwa sasa ujenzi umeanza.

Akiwa Butiama, Mhe. Majaliwa pia amefanya kikao na watumishi na madiwani, ametembelea nyumbani kwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na kupokelewa na wanafamilia, amewasalimia wananchi na kuendelea na ziara yake Wilaya ya Serengeti.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.