• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Maandalizi ya Sensa Yakamilika

Posted on: August 23rd, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mzee ameeleza kuwa maandalizi ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 katika Mkoa wa Mara yamekamilika.

Akizungumza katika matangazo ya moja kwa moja yaliyorushwa kupitia Kituo cha Redio cha Bunda FM leo, Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa tayari Makarani wa Sensa wapo katika maeneo yao ya kazi na wanaendelea na maandalizi ya kuanza zoezi saa sita usiku wa kuamkia kesho tarehe 23 Agosti, 2022.  

“Maandalizi yote muhimu ya Sensa kwa Mkoa wa Mara yamekamilika, na tayari makarani wapo katika vituo na Wasimamizi wa Sensa wanaendelea kupokea changamoto na kuzitatua kwa kadiri zinavyoendelea kutolewa katika maeneo mbalimbali” alisema Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa kwa mujibu wa Sheria ya Takwimu sura ya 351, taarifa zote zitakazotolewa na wananchi kwa karani wa Sensa zitakuwa ni siri na zitatumika kwa madhumuni ya Sensa na makarani wote wamesaini kiapo cha kutunza siri za taarifa zote atakazozikusanya katika zoezi la Sensa.

“Karani yeyote akithibitika kwenda kinyume na kiapo cha kutunza siri, atashtakiwa na kuadhibiwa kwa mujibu wa sheria hii, hivyo ninaomba kuwahakikisha wananchi kuwa taarifa watakazozitoa kwa karani wa Sensa zipo salama na hivyo niwaombe watoe taarifa sahihi ili Serikali ipate takwimu sahihi” alisema Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee ambaye aliambatana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu, ameeleza kuwa makarani wa sensa wakienda kuhesabu watu wataambatana na viongozi wa serikali ya mtaa au vitongoji wa eneo husika.

Mheshimiwa Mzee amewaomba wananchi wote wa Mkoa wa Mara kushiriki kikamilifu katika zoezi la Sensa ya Watu na Makazi la mwaka 2022, kutoa taarifa sahihi kwa makarani wa Sensa na wazazi/walezi wa Watoto/watu wenye ulemavu kuhakikisha watu wote wenye ulemavu wanahesabiwa.

 “Hii itaiwezesha Serikali kutambua idadi ya watu wenye ulemavu katika kila eneo, aina ya ulemavu, msaada unaohitajika na namna bora ya kuweza kuwasaidia mmoja mmoja au kama kundi la watu wenye ulemavu” alisema Mheshimiwa Mzee.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • RC atoa siku 14 wanafunzi wote Sekondari ya J. K. Nyerere wapate chakula shuleni

    July 28, 2025
  • Kusaya apokea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama

    July 25, 2025
  • Mtambi ataka matumizi ya GOTHOMIS kwa asilimia 100 Mara

    July 25, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.