• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Maadhimisho ya Siku ya Ukimwi yafana

Posted on: December 19th, 2023

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani katika Mkoa wa Mara yamefanyika leo Desemba 1, 2023 katika eneo la Kisorya, Wilaya ya Bunda huku kauli mbiu ikiwa Jamii Iongoze Kutokomeza UKIMWI.

Akizungumza katika maadhimisho hayo, mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Bunda Dkt. Vincent Anney amesema siku hii ni maalum kwa ajili ya kukumbushana kuwa UKIMWI bado upo tuchukue tahadhari.

Dkt. Anney ameeleza kuwa kwa sasa zana za kupambana na UKIMWI zipo na zinapatikana katika maeneo mengi mijini na vijijini na kwa sasa vipimo ili kujua hali ya afya vinatolewa bure.

Amezitaja Halmashauri zenye maambukizi makubwa kuwa ni pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Musoma 3.8; Halmashauri ya Wilaya ya Rorya 3.6 na wastani wa Mkoa wa Mara kuwa ni 2.1.

Mhe. Dkt. Anney ameeleza kuwa kila mmoja akitimiza wajibu wake, maambukizi ya UKIMWI yatapungua na hata kuisha kabisha.

Amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha kuwa Kamati za Ukimwi za Kata, Vijiji  na ngazi ya Halmashauri zinafanyika na mihutasari ya vikao hivyo inawasilishwa kwenye mamlaka husika ili kupata taarifa ya masuala yaliyojiri katika vikao hivyo.

Amewashukuru wadau mbalimbali ambao wamejitoa kuusaidia Mkoa wa Mara katika mapambano dhidi ya UKIMWI kwa kuimarisha utoaji wa huduma, vifaa tiba na miundombinu ya sekta ya afya.  

Kwa upande wake, Kaimu Katibu Tawala Sehemu ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii Dkt. Omari Gamuya ameeleza kuwa kwa sasa Mkoa una watu 66,436 wanaoishi na VVU na kati yao 64,315 wanatambua hali yao ya maambukizi .

Dkt. Gamuya ameeleza kuwa kati ya wote wanaojua kuhusu hali zao za maambukizi wanaume ni 20,109 na wanawake ni 44,206 wakati watoto ni 2137 na wakati watu wanaojua hali zao za maambukizi 61,099 wameanza kutumia dawa.

Ameeleza kuwa Mkoa wa Mara una jumla ya vituo vya tiba na mafunzo 174 na vituo vya tohara kinga ya kitabibu kwa wanaume 34.

Kwa mujibu wa Dkt. Gamuya, kwa mwaka 2022/2023 Mkoa wa Mara kwa kushirikiana na wadau umesambaza mipira ya kiume (kondomu) 2,153,740 na kutoa elimu katika maeneo mbalimbali.

 Maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani yamehudhuriwa na viongozi wa Wilaya ya Bunga, maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, Wawakilishi kutoka Halmashauri zote za Mkoa wa Mara, wadau na wananchi.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.