• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

LAAC yaipongeza Manispaa ya Musoma

Posted on: March 24th, 2024

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) leo imefanya ziara katika Halmashauri ya Manispaa ya Musoma ambapo imetembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya Rwamlimi na Shule ya Sekondari ya Kigera Mwiyale na kuipongeza Manispaa hiyo kwa usimamizi mzuri wa mradi.

Akizungumza katika kikao cha majumuisho, Makamu Mwenyekiti wa LAAC Mhe. Stanslaus Mabula ambaye ameongoza msafara huo, ameipongeza Manispaa ya Musoma kwa usimamizi mzuri wa mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya Rwamlimi.

“Ujenzi wa Shule ya Sekondari (Kigera Mwayale) ukamilike mapema iwezekanavyo, madarasa yawekewe vigae na gharama za nyongeza katika majengo yanayohitaji ukamilishaji ziendane na uhalisia kulingana na kazi iliyobakia” amesema Mhe. Mabula.

Aidha, Mhe. Mabula ameitaka Manispaa ya Musoma kujibu hoja za ukaguzi zilizoibuliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Fedha za Serikali (CAG) katika Mwaka wa fedha 2021/2022 na kuwasilisha majibu hayo kwa Mkaguzi kabla ya Septemba, 2024.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Manispaa ya Musoma Bwana Bosco Ndunguru ametoa ufafanuzi kuhusiana na hoja mbalimbali zilizoibuliwa na wabunge katika kikao cha majumuisho.

Bwana Ndunguru ameeleza kuwa fedha za Shule hiyo zilikuja kwa ajili ya Kata ya Kwangwa ambayo awali kabla ya kugawanywa ilikuwa ni kata moja na Kigera na Uongozi wa Manispaa ulibadilisha matumizi ya fedha hizo ili kujenga shule Kata ya Kigera ambayo ilikuwa haina Shule ya Sekondari.

“Maamuzi haya yamesaidia sana kupunguza idadi ya wanafunzi katika shule ya Kwangwa na kuwapunguzia umbali wanafunzi wa Kigera kwenda Kwangwa na badala yake kwa sasa wanasoma katika Shule ya Sekondari ya Kigera Mwiyale” amesema Bwana Ndunguru.

Bwana Ndunguru ameeleza kuwa Halmashauri kupitia mapato ya ndani imelipa fidia kwa wananchi milioni 82 ili kuweza kupata eneo la kujenga shule hiyo na imetenga fedha shilingi milioni 200 katika bajeti ya mwaka 2024/2025 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa nane katika shule hiyo.

Aidha, Bwana Ndunguru amesema Manispaa imeomba shilingi milioni 153 kwa ajili ya ukamilishaji wa majengo ya shule hiyo baada ya fedha zilizopokelewa shilingi milioni 470 kuisha na baadhi ya majengo yakiwa hayajakamilika.

Awali, wakitoa michango yao, baadhi ya wabunge mbali na kupongeza ujenzi wa miradi hiyo waliomba ufafanuzi kuhusiana na kwa nini fedha ilibadilishiwa kata ya kujenga mradi kutoka Kata ya Kwangwa hadi Kata ya Kigera na mchango wa Halmashauri katika ujenzi wa mradi wa Shule ya Sekondari ya Kigera Mwiyale.

Ziara hiyo imehudhuriwa pia na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Meya wa Manispaa ya Musoma, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Musoma, maafisa kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, Wizara ya Fedha, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na Manispaa ya Musoma.

Kesho, Kamati ya LAAC itatembelea na kukagua miradi katika Halmashauri ya Wilaya ya Butiama ambapo itatembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Kamugegi na Hospitali ya Wilaya ya Butiama.  

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.