• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Kusaya awataka Wakurugenzi kuongeza bajeti ya Ustawi wa Jamii

Posted on: July 22nd, 2024

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Gerald Musabila Kusaya leo tarehe 19 Julai, 2024 ameongoza kikao cha tathmini ya Programmu Jumuishi ya MAlezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto na kuwataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuongeza bajeti ya Vitengo vya Ustawi wa Jamii ili viweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

Bwana Kusaya amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kutenga magari kwa ajili ya Maafisa Ustawi wa Jamii ili waweze kufuatilia kwa ukaribu changamoto za wananchi na hususan watoto katika maeneo mbalimbali wanayofanyia kazi.

“Tukiviwezesha Vitengo vya Ustawi wa Jamii tutapunguza wananchi wenye kero wanaokuja kuwaona viongozi kwa kero mbalimbali, kwa sababu Maafisa Ustawi wa Jamii watazipunguza baadhi ya kero hizo” amesema Bwana Kusaya.

Bwana Kusaya pia amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha programu hii inazinduliwa katika ngazi za Kata, Mtaa na Vijiji katika Halmashauri zote na kuipongeza Halmashauri ya Mji wa Tarime kwa kufanikiwa kuzindua programu hiyo katika Kata zake zote nane za Halmashauri hiyo.

Bwana Kusaya amesema programu hii inawaleta pamoja wadau wa maendeleo wa sekta mbalimbali ili waweze kufanyakazi kwa ushirikiano katika kuhakikisha watoto wenye umri wa miaka 0-8 wanapata huduma za malezi jumuishi, wanastawi na kufikia hatua za ukuaji timilifu.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara amesema programu hii inatekelezwa katika vipengele vikuu vitano ambavyo ni lishe toshelevu, malezi yenye mwitikio, ulinzi na usalama, afya bora na fursa za ujifunzaji wa awali.

Kwa upande wake, Bibi Mary Shillah Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Makundi Maalum ameupongeza Mkoa wa Mara kwa uwakilishi mzuri wa maafisa wa Serikali na wadau wengi kujitokeza katika kikao hicho.  

Bibi Shillah ameeleza kuwa Serikali imeamua kufuatilia watoto katika umri wa miaka 0-8 kwa sababu wataka wadau wengine waongezeke kama vile Benki ambazo zina akaunti maalum za watoto,

Kwa upande wake, Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Mara Bi. Elizabeth Mahinya amewaomba Wakurugenzi wa Halmashauri kuongeza bajeti ya Vitengo vya Ustawi wa Jamii ili vitengo hivyo viweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi katika kuihudumia jamii.

Bi. Mahinya amesema watendaji waliopo wanaweza kutekeleza majukumu yao vizuri lakini wanakwamishwa na bajeti zinazotengwa katika vitengo hivyo katika kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Aidha, Bi. Mahinya amewataka Maafisa Ustawi wa Jamii kufanyakazi kwa ushirikiano ili kwa umoja wao waweze kupata matokeo makubwa katika kuwahudumia wananchi.

Programu Jumuishi ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto ilianza kutekelezwa mwaka 2021/2022- 2025/2026 na ilizinduliwa rasmi tarehe 13 Desemba, 2021 katika Jiji la Dodoma na Mhe. Doroth Gwajima Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Makundi Maalum.

 Kikao hicho kimehudhuriwa na Makatibu Tawala wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Maafisa Ustawi wa Jamii na wadau mbalimbali wanaoshirikiana na Halmashauri katika kutekeleza programu hiyo katika Mkoa wa Mara.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.