• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Kusaya akagua maendeleo ya ujenzi MJNUAT

Posted on: May 15th, 2024

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Gerald Musabila Kusaya leo tarehe 14 Mei, 2024 amefanya ziara katika Wilaya ya Butiama ambapo amekagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa Chuo Kikuu cha Mwalimu Julius K. Nyerere cha Kilimo na Teknolojia (MJNUAT), Butiama.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa mradi huo, Bwana Kusaya ameitaka Menejimenti ya Chuo cha MJNUAT na Mshauri welekezi wa mradi huo kusimamia kikamilifu na kuhakikisha kuwa mradi huo unakamilika kwa wakati na kwa ubora.

“Huu mradi unapaswa kukamilika mapema kulingana na mikataba yake ili watu waweze kuanza kupata huduma za elimu kwa wakati na utekelezaji wake uzingatie viwango vya ubora vya majengo haya” amesema Bwana Kusaya.

Majengo yanayojengwa katika mradi huo ni Chuo cha Kilimo, Skuli ya Kilimo, usindikaji na Teknolojia, Skuli ya Uhandisi na Teknolojia ya Nishati na Madini, jengo la utawala, barabara na njia za kupita, mabweni, cafeteria, maabara na kalakana za uhandisi na kilimo kwa gharama ya shilingi bilioni 102.5.

Mradi huo unaotekelezwa na wakandarasi mbalimbali unategemewa kutekelezwa kwa muda wa miezi 18 kuanzia Novemba, 2023 na unapaswa kukamilika ifikapo Mei, 2025 na kwa sasa umefikia wastani wa asilimia 18. 5 ya utekelezaji wake.

MJNUAT ni moja kati ya taasisi 22 za Elimu ya Juu nchini Tanzania zilizonufaika na mradi wa Higher Education for Economic Transformation (HEET) unaofadhiliwa na Benki ya Dunia.

Mradi wa HEET una lengo la kuboresha miundombinu na mifumo ya kitaasisi ya Vyuo vya elimu ya Juu hapa nchini na unatekelezwa kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia 2021-2026.  

 Katika ziara hiyo, Katibu Tawala aliambatana na baadhi ya maofisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na Menejimenti ya Chuo cha MJNUAT.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • RC atoa siku 14 wanafunzi wote Sekondari ya J. K. Nyerere wapate chakula shuleni

    July 28, 2025
  • Kusaya apokea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama

    July 25, 2025
  • Mtambi ataka matumizi ya GOTHOMIS kwa asilimia 100 Mara

    July 25, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.