• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

KU yakagua miradi ya Mwenge Serengeti na Tarime

Posted on: July 12th, 2024

Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mara inayoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 11 Julai, 2024 imekagua miradi itakayotembelewa na Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2024 katika Wilaya za Serengeti na Tarime.

Kamati ikiwa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti imekagua ujenzi wa soko la Kijiji cha Makundusi linalojengwa kwa mapato ya Kijiji hicho na Barabara ya Parknyigoti hadi Nichoka pamoja na ujenzi wa daraja.

Kamati ikiwa katika Halmashauri hiyo, imepokea taarifa ya miradi yote itakayotembelewa na Mwenge wa Uhuru na taarifa ya utekelezaji wa maagizo yote yaliyotolewa na Kamati ya Wataalamu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, Kamati ilikagua mradi wa jengo la kitega uchumi la Nyamongo Plaza linalomilikiwa na Bwana Josephati Mwita pamoja na mradi wa maji wa Nyangoto ambao ulitekelezwa kwa ufadhiri wa Mgodi wa Barrick North Mara na ulizinduliwa na Mwenge wa Uhuru na kwa mwaka huu utaenda kuangalia uendelezaji wake.

Katika Halmashauri ya Mji wa Tarime, Kamati ilikagua mradi wa ujenzi wa Shule ya Msingi Kede ambayo imejengwa kwa fedha za Serikali, mchango wa wananchi na mchango wa Halmashauri ya Mji wa Tarime na Daraja la Kinyambi katika mto Moi linalojengwa na Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA).

Ikiwa katika Wilaya ya Tarime, Kamati imepokea taarifa ya miradi yote itakayotembelewa na Mwenge wa Uhuru na taarifa ya utekelezaji wa maagizo yaliyotolewa na Kamati ya Wataalamu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Kamati iliziagiza Halmashauri hizo kutekeleza maagizo yote yaliyotolewa na kuandaa hamasa kubwa wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru katika Halmashauri hizo.

Kamati ya Usalama ya Mkoa iliambatana na Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Serengeti na Wilaya ya Tarime, wataalamu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na Halmashauri za Tarime DC, Tarime TC na Serengeti DC.

Mwenge wa Uhuru unatarajiwa kupokelewa katika Mkoa wa Mara tarehe 26 Julai, 2024 ukitokea Mkoa wa Arusha na utakimbizwa katika Halmashauri zote tisa za Mkoa wa Mara hadi tarehe 4 Agosti, 2024 utakapokabidhiwa katika Mkoa wa Simiyu.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.