• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Kituo cha Afya Genkuru kilichotumia milioni 700 hakijakamilika

Posted on: August 16th, 2021

Mradi wa upanuzi wa Zahanati ya Kijiji cha Genkuru katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime uliotengewa zaidi ya milioni 700 haujakamilika huku fedha zikitumika kununua vifaa vingi vilivyobakia stoo.

Hayo yamebainika leo tarehe 13 Agosti 2021 katika ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Mara aliyoifanya katika mradi huo unaojengwa kwa fedha za uwajibikaji kwa jamii zilizotolewa na Mgodi wa Dhahabu wa North Mara mwaka 2018.

Kufuatia tatizo hilo Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ameagiza kukamatwa kwa watu wote waliohusika kwa namna moja au nyingine na mradi huo ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yao.

“Nawaagiza Polisi na TAKUKURU kukamata watu wote wanaohusika na mradi huu ili waweze kuzirejesha fedha zilizotumika vibaya katika mradi huu” alisema Mheshimiwa Hapi.

Akikagua mradi huo Mheshimiwa Hapi ameshuhudia vifaa vingi vikiwa vipo stoo na vingine kama vile matofali, karatasi za kuzuia maji, vigae, nondo na mabati vikiwa vimebakia kwa wingi lakini havihitajiki tena.

Mheshimiwa Hapi amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime kuchunguza uhalili wa matumizi ya fedha nyingine ambazo zililetwa katika kijiji hicho.

Fedha hizo ni shilingi milioni 100 zinazodaiwa kupelekwa kijiji kingine; milioni 37 zinazodaiwa kulipa mawakili waliosimamia kesi; milioni 15 zinazodaiwa kulipa wadhamini wa kesi; huku milioni 18 zikilipwa viongozi wa kijiji waliokuwa wanahudhuria kesi Mahakama Kuu, Mwanza.

Kwa upande wake Mtendaji wa Kijiji cha Genkuru Bwana Gichovu Chacha  ameeleza kuwa vifaa vilivyonunuliwa vilitokana na maelekezo waliyopewa na Afisa Mununuzi na Mhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime ambao ndio walikuwa wataalamu katika utekelezaji wa mradi huo.

Bwana Chacha ameyataja majengo yaliyojengwa katika mradi huo kuwa ni cliniki ya Baba, Mama na Mtoto (RCH), jengo la Mama na Mtoto, jengo la upasuaji, mochwari, maabara na nyumba moja pacha ya watumishi, choo cha matundu manne.

Mtendaji huyo ameeleza kuwa hamna jengo hata moja lililokamilika baada ya fedha nyingi kutumika kununua vifaa ambavyo havihitajiki tena katika mradi huo huku fedha za kukamilisha mradi huo zikiwa hamna.

 Wakizungumza na Mkuu wa Mkoa wananchi wa kijiji hicho wameeleza kuwa huu ni mwaka wa kumi uongozi wa kijiji chao hauwapi taarifa za mapato na matumizi ya kijiji chao.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.