• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Kanali Mtambi akabidhiwa ofisi Mara

Posted on: April 9th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mohamed Mtanda leo amekabidhi ofisi kwa Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi katika hafla fupi iliyofanyika katika Ukumbi wa Uwekezaji, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Akizungumza katika hafla hiyo, Kanali Mtambi amewataka viongozi na watumishi wa umma wa Mkoa wa Mara kutimiza wajibu wao kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za uongozi na utumishi wa umma na kuweka kipaumbele katika kuwahudumia wananchi.

“Lengo ni kuhakikisha kuwa tunatimiza wajibu wetu wa kuwatumikia wananchi na kutatua changamoto zao kwa nafasi zetu tulizonazo, sitavumilia uzembe wa aina yoyote na kutoka kwa mtu yoyote” amesema Mhe. Kanali Mtambi.

Aidha, amezitaka taasisi zinazotakiwa kutoa huduma saa 24 kwa siku kuhakikisha zinatoa huduma kikamilifu muda wote ikiwemo hospitali, jeshi na polisi kuhakikisha wanaboresha pia huduma zinazotolewa usiku na siku za mwishoni mwa wiki.

“Kuna hii tabia ukienda hospitali usiku au siku za mwisho wa wiki unaambiwa huwezi kupata vipimo au mtaalamu Fulani hayupo mgonjwa anaambiwa njoo siku nyingine, hili halikubaliki Mkoa wa Mara” amesema Mhe. Mtambi.

Amezitaka Mamlaka za Serikali za Mitaa kufuata sheria, taratibu na kanuni katika kutekeleza miradi ya maendeleo ili iweze itekelezwe kwa ubora na ikamilike kwa wakati unaotegemewa ili wananchi wapate huduma katika miradi hiyo.

Mhe. Mtambi amesema anataka kupunguza uhalifu katika Mkoa wa Mara na kumtaka Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mara kuwashughulikia wahalifu kabla hawajafanya uhalifu na kumtaka kufufua mifumo  ya kiintelijensia ifanye kazi ya kubaini uhalifu kabla haujatokea.

Amemwagiza Mkuu wa Wilaya ya Musoma kuhakikisha mlipuko wa kuharisha na kutapika ulioanza katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma unadhibitiwa na hauenei katika Mkoa wa Mara na kufanya ukaguzi wa usafi wa mazingira mara kwa mara.

Amewaagiza mameneja wa Mkoa wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) na Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) kuhakikisha kuwa barabara na madaraja yote yanapitika muda wote pamoja na  mvua zinazoendelea kunyesha.

Amezitaka Mamlaka na wakala za Maji katika Mkoa wa Mara kuhakikisha huduma ya maji inapatikana kwa wananchi na miradi ya maji inakamilika kwa wakati na kutoa huduma kwa wananchi ili kuwawezesha wananchi kufanya shughuli nyingine za maendeleo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mohamed Mtamba amewashukuru viongozi,  watumishi na wananchi wa Mkoa wa Mara kwa ushirikiano mkubwa waliompatia wakati wote akiwa Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Mhe. Mtanda ameeleza kuwa pamoja na mambo mengine yanayosikika kuhusu Mkoa wa Mara kwa watanzania wengine, wananchi wa Mkoa wa Mara ni watu wema, wakarimu na wanapenda maendeleo yao.

Mhe. Mtanda amempongeza Mhe. Mtambi kwa kuaminiwa na kuteuliwa kuuongoza Mkoa wa Mara na kuwataka watu wa Mkoa wa Mara kumpa ushirikiano ili aweze kutekeleza majukumu yake kikamilifu.  

Hafla ya makabidhiano imehudhuriwa na viongozi wa dini, viongozi wa vyama vya siasa, Wakuu wa Wilaya, Kamati ya Usalama ya Mkoa, Meya wa Manispaa ya Musoma, Wakuu wa Sehemu na Vitengo vya Sekretarieti ya Mkoa wa Mara, Makatibu Tawala wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, wakuu wa taasisi za umma, wafanyakazi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.