• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara kuanza kutoa huduma Aprili 2020

Posted on: March 6th, 2020

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara ya Kwangwa inatarajia kuanza kutoa huduma katika Jengo la Mama na Mtoto kuanzia tarehe 17 Aprili 2020 baada ya kukamilika ujenzi wa upande huo na huduma zote muhimu za kuwezesha kuanza kufanya kazi.

Hayo yameelezwa leo baada ya kikao cha pamoja kati ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mheshimiwa Ummy Mwalimu, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa William Lukuvi na Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kigoma Malima, wawakilishi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ambao ndio wakandarasi na mwakilishi wa Chuo Kikuu cha Ardhi ambaye ni Mshauri Mwelekezi katika mradi huo pamoja na maafisa waandamizi wa serikali.

Akizungumza baada ya kikao hicho Mheshimiwa Lukuvi ameeleza kuwa amewaagiza NHC kuhakikisha kuwa wanafanyakazi ya kukamilisha ujenzi wa hospitali hii kwa usiku na mchana na kuhakikisha kuwa huduma zitaanza kutolewa kwa muda uliopangwa.

 “Kwa sasa Mshauri Mwelekezi anarekebisha michoro ya awali ya majengo hayo ili iweze kukidhi mahitaji yote ya msingi ya majengo ya wakati huu” alisema Mheshimiwa Lukuvi.

Kwa upande wake Mheshimiwa Mwalimu amesema kuwa wanategemea kuwa hospitali hii itaanza kufanyakazi kwa kutoa huduma za mama na mtoto na makubaliano ni kuwa hadi kufikia Julai, 2020 hospitali yote itakuwa imekamilika kutoa huduma kwa wananchi.

“Tunategemea kuwa ujenzi huu ukikamilika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara itahamia hapa Kwangwa na pale ilipo sasa yale majengo yatatumika kama Hospitali ya Manispaa ya Musoma” alisema Mheshimiwa Mwalimu

Aidha amesema kuwa hospitali hii haitakuwa hospitali ya Rufaa ya Mkoa bali itakuwa ni hospitali ya kibingwa na kibobezi kwa baadhi ya huduma na itatoa huduma kwa wananchi wote wa Kanda ya Ziwa.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mheshimiwa Adam Kighoma Malima amesema kuwa ziara ya viongozi hawa imesadia sana katika kutatua changamoto zilizokuwa zinaukabili ukamilishaji wa hospitali hii. 

Ujenzi wa Hospitali ya Kwangwa ulianza mwaka 1977 na ulikuwa ukijengwa taratibu hadi mwaka 2018 ambapo Rais wa awamu ya tano Mheshimiwa Dokta John Pombe Joseph Magufuli alipoamua kutoa shilingi bilioni 15 kwa ajili ya kumalizia ujenzi huu.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • RC atoa siku 14 wanafunzi wote Sekondari ya J. K. Nyerere wapate chakula shuleni

    July 28, 2025
  • Kusaya apokea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama

    July 25, 2025
  • Mtambi ataka matumizi ya GOTHOMIS kwa asilimia 100 Mara

    July 25, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.