• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Hapi awataka wakufunzi wa Sensa kuwa mfano

Posted on: July 29th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi amewataka wakufunzi wa Sensa ya Watu na Makazi, 2022 kuwafundisha na kuwa mfano mzuri kwa wasimamizi na makarani wa sensa katika Halmashauri zao ili kufanikisha zoezi la Sensa katika Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Hapi ametoa agizo hilo leo tarehe 26 Julai, 2022 wakati alipokuwa anafunga mafunzo ya sensa kwa wakufunzi wa sensa ngazi ya Mkoa yaliyofanyika katika Chuo cha Maendeleo ya Jamii Buhare katika Manispaa ya Musoma.

“Serikali imetumia fedha nyingi kugharimia maandalizi ya Sensa hii, ninatambua pia kwa mwaka huu wengi wa makarani sio waajiriwa wa serikali, na hivyo ninaomba mkawafundishe kufanya kazi hii kwa uadilifu na kufuata miiko, taratibu na matakwa ya kazi hii” alisema Mheshimiwa Hapi.

Aidha, Mheshimiwa Hapi amewaeleza wakufunzi hao kuwaelekeza wasimamizi na makarani wa sensa kuepuka masuala binafsi, tofauti za kisiasa, itikadi na kidini wakati wa kutekeleza zoezi la Sensa ili kuleta ufanisi wa zoezi hilo.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa sensa ni zoezi muhimu sana kwa Taifa kwa kuwa taarifa zitakazopatikana zitaisaidia serikali katika kupanga mipango ya maendeleo ya wananchi kwa kuzingatia mahitaji halisi.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa amewataka waratibu wa Sensa kuhakikisha kuwa makarani wa sensa wanapata malipo yao kwa wakati ili kurahisisha utekelezaji wa shughuli za sensa kwa ufanisi.

“Ni vizuri makarani wote na wasimamizi na wahusika wengine wote kwenye zoezi la sensa wapate malipo yao kwa wakati ili kurahisisha utekelezaji wa zoezi la kukusanya taarifa kutoka kwa wananchi kwa ukamilifu” alisema Mheshimiwa Hapi.

Aidha, amewaomba Waandishi wa Habari kuendelea kupeleka taarifa za sensa kwa wananchi ili wananchi waweze kupata taarifa sahihi na kushiriki kikamilifu katika zoezi hilo tarehe 23 Julai, 2022.  

Kwa upande wake, Mratibu wa Sensa Mkoa wa Mara Bwana David Danda ameeleza kuwa mafunzo ya wakufunzi wa sensa ngazi ya Mkoa yamefanyika kwa siku 21 kuanzia tarehe 6 Julai, 2022 na kuwahusisha wakufunzi 296 kutoka Halmashauri zote za Mkoa wa Mara.

Bwana Danda ameeleza kuwa mpaka leo wakufunzi hao wamefundishwa, kufanya mitihani na kufuzu mafunzo yao na sasa wapo tayari kwa ajili ya kwenda kuwaelimisha wasimamizi na makarani wa sensa 69,000 ambao wamechaguliwa kutoka Halmashauri zote za Mkoa wa Mara.

 Sensa ya Watu na Makazi kwa mwaka 2022 inatarajiwa kufanyika hapa nchini tarehe 23 Agosti, 2022 na kuwahusisha watu wote watakaolala hapa nchini usiku wa kuamkia tarehe 23 Agosti, 2022.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.