• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Hapi awapongeza Wanamara

Posted on: February 17th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi amewapongeza wananchi wa Mkoa wa Mara kwa ushirikiano, utulivu, uzalendo na mshikamano walioionyesha wakati wote ambapo Mkoa ulipata ugeni mkubwa wa viongozi wa Chama cha Mapinduzi na Serikali walioshiriki katika maadhimisho ya miaka 45 ya CCM na ziara ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.  

Akizungumza katika kikao cha tathmini ya miradi ya maendeleo kilichofanyika leo tarehe 15 Februari 20222 katika ukumbi wa uwekezaji uliopo katika Ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mheshimiwa Hapi amesema wananchi walionyesha uzalendo wa hali ya juu.  

“Wananchi walihakikisha kuwa ziara ya Mheshimiwa Rais inafanyika kwa amani, utulivu na hamasa kubwa sana, kwa niaba ya viongozi wote wa Mkoa wa Mara ninawapongeza sana” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi amewataka wananchi kuendelea na uzalendo huo kwa manufaa ya wananchi wenyewe lakini na taifa kwa ujumla.

Aidha amevipongeza vyombo vya usalama kwa kusimamia amani na utulivu katika maeneo yote ya Mkoa wa Mara na kuhakikisha wageni wote wanarudi majumbani kwao wakiwa salama.

Mheshimiwa Hapi pia amewashukuru wafanyabiashara wa Mkoa wa Mara ambao walitoa huduma mbalimbali kwa wageni waliokuja na kuujengea sifa Mkoa wa Mara.

“Wafanyabiashara wengi waliitikia wito wa kufanya biashara zao saa 24 kwa siku ambazo wageni walikuwepo katika Mkoa wa Mara, hii ilisaidia kutoa huduma kwa wageni ambao walichelewa kufika na ambao walihitaji kuamka mapema kuwahi sehemu mbalimbali.

Aidha, Mheshimiwa Hapi amewataka wafanyabiashara wa Mkoa wa Mara kuendelea kuboresha huduma katika biashara zao kwa kuwa wageni wameondoka na sifa nzuri za Mkoa wa Mara wengine watapenda kuja tena wakati mwingine wakute huduma bora zaidi.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa kujitokeza kwa wananchi kwenye mikutano na maeneo ambayo Mheshimiwa Rais alikuwa anapita ni ishara nzuri kuwa wananchi wengi wanaipenda serikali yao.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alifanya ziara ya siku nne katika Mkoa wa Mara ambapo alikuwa Mgeni Rasmi wa Maadhimisho ya miaka 45 ya Uhuru, aliweka jiwe la msingi katika mradi wa maji wa Mgango- Kiabakari- Butiama, alitembelea Hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (Kwangwa) na kuweka jiwe la msingi katika mradi wa maji Bunda.

Aidha katika ziara hiyo Mheshimiwa Rais alizungumza na wananchi katika Uwanja wa Karume uliopo Manispaa ya Musoma, eneo la Mgango, Kwangwa, Butiama na Mji wa Bunda.

Katika ziara hiyo Mheshimiwa Rais pia alitembelea nyumbani kwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika eneo la Mwitongo ambapo pamoja na mambo mengine alizuru na kuweka Shada la Maua katika kaburi la Baba wa Taifa.  

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.