• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Hapi awaongoza Wananchi Kusherekea Muungano

Posted on: April 26th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara leo amewaongoza wananchi wa Wilaya ya Musoma kupanda miti 1,000 katika Shule ya Sekondari ya Kiara kama sehemu ya Maadhimisho ya miaka 58 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Akizungumza baada ya zoezi la upandaji miti, Mheshimiwa Hapi amewataka wananchi wa Mkoa wa Mara kupanda miti ili kulinda mazingira ya Mkoa wa Mara kwa ajili ya vizazi vijavyo.

“Miti hii ambayo kivuli chake tunakipata leo, ilipandwa na wazee wetu hapo zamani na sasa ni wajibu wetu kupanda miti na kutunza mazingira” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi amewataka wanafunzi na walimu wa shule zote za Mkoa wa Mara kupanda miti katika maeneo yao ili kulinda uoto wa asili wa Mkoa wa Mara.

Akitoa shukrani kwa Mkuu wa Mkoa, Meya wa Manispaa ya Musoma Mheshimiwa William Gumbo ameeleza kuwa Shule ya Sekondari ya Kiara imechaguliwa kuzindua zoezi la upandaji miti kutokana na sababu za kihistoria.

“Serikali ilipoanza kujenga shule za kata, shule ya kwanza kujengwa na wananchi wa Manispaa ya Musoma ilikuwa ni Sekondari ya Kiara, mwitikio ulikuwa mkubwa sana na nguvu za wananchi zilifanikisha ujenzi wa shule nzima ndani ya muda mfupi” alisema Mheshimiwa Gumbo.

Mheshimiwa Gumbo ameeleza kuwa hata zoezi hili la upandaji wa miti linaweza kufanikiwa sana kutoakana na uzoefu huo na mwitikio wa wananchi katika ujenzi wa Shule hiyo.

Mstahiki Meya amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kuungana na wananchi wa Manispaa ya Musoma kupanda miti kama sehemu ya uzinduzi wa kampeni ya kupanda miti 30,000 katika Manispaa ya Musoma.

Mheshimiwa Gumbo ameeleza kuwa zoezi la kupanda miti katika Manispaa ya Musoma ni endelevu na kuwataka wanafunzi na wananchi kuchukua miche ya miti katika kitalu cha Wakala wa Misitu (TFS) Manispaa ya Musoma na kupanda katika maeneo yao.

Zoezi la kupanda miti lilihudhuriwa pia na Kamati ya Usalama ya Mkoa, Katibu Tawala wa Wilaya ya Musoma, Wakuu wa Idara na Vitengo wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, wakuu wa taasisi za serikali na wafanyakazi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Wengine waliohudhuria ni Meya wa Manispaa ya Musoma, Mkurugenzi wa Manispaa ya Musoma, Wakuu wa Idara na Vitengo vya Manispaa ya Musoma na watumishi wa Manispaa ya Musoma, wanafunzi na walimu wa Shule ya Sekondari ya Kiara.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.