• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Hapi awahimiza viongozi wa dini kuhubiri amani

Posted on: June 16th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi leo amekutana na viongozi wa dini wa Mkoa wa Mara na kuwataka viongozi hao katika mahubiri yao kuhimiza umoja, amani na usalama.  

“Ninawaomba viongozi wa dini mkemee watu kutembea na silaha kila wakati bila ya sababu za msingi na matokeo yake mtu amemkosea kidogo tu anamfanyia ukatili wa kutisha jambo ambalo halipendezi” alisema Mheshimiwa Hapi.  

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa hivi sasa kumekuwa na matukio mengi ya ukatili katika jamii ambayo yanaashiria kuna sehemu jamii imepotoka na inahitaji kujirekebisha katika masuala ya maadili na kumjua Mungu na kuwataka viongozi hao kuendelea kutoa mafundisho ya kukemea ukatili kwa waumini wao.

Amewahamasisha viongozi hao wa dini kutumia nafasi zao na kukemea masuala yote ambayo yanadhalilisha wanawake, watoto na makundi yenye mahitaji maalum katika jamii kwa kukemea vitendo vya ukeketaji, baadhi ya mila potofu na mahusiano mabaya katika jamii.

Mheshimiwa Hapi amewataka viongozi wa dini kuhimiza malezi bora ya watoto na msingi mzuri wa familia ili kuweza kuwalinda waumini wao dhidi ya watu wasio na maadili mema kutoa elimu kwa makundi mbalimbali na hatimaye kubomoa jamii.

Amewataka viongozi wa dini kuisaidia Serikali katika kulinda amani na utulivu wa nchi ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa pale ambapo wanahisi kunatatizo kwa vyombo vya usalama ili kuweza kulinda amani na utulivu uliopo nchini.  

Mheshimiwa Hapi ameitaka Ofisi ya Kamishna wa Ardhi Mkoa wa Mara kutumia hekima katika kudai kodi ya ardhi ikiwa ni pamoja na kuwasiliana na viongozi wa dini kabla ya kuwapelekea madai ya kodi ya ardhi au kukumbushia malipo ya kodi ya ardhi.

Amewaagiza Wakuu wa Wilaya kufuatilia Mamlaka ya Udhibiti ya Usafiri Ardhini (LATRA) kuhusiana na kupanda kwa nauli katika maeneo mbalimbali hapa mkoani kulingana na hali halisi ya bei za mafuta zilivyo kwa sasa.

Risala ya viongozi wa dini kwa Mkuu wa Mkoa pamoja na masuala mengine ilimuomba Mkuu wa Mkoa kuwasaidia katika masuala ya kodi ya ardhi na kuwaombea msamaha wa malimbikizo ya kodi ya ardhi ya miaka ya nyuma ambapo walipatiwa utaratibu wa kufuata ili kuweza kulishughulikia suala hilo.

Aidha viongozi hao wamelalamikia tozo wanazolipa wanapoomba vibali kwa ajili ya mihadhara ya kidini katika mamlaka mbalimbali za Serikali na mfumko wa bei ambapo kwa kiasi kikubwa unawatesa wananchi katika kupata mahitaji yao muhimu.  

Viongozi hao wamemuomba Mkuu wa Mkoa kuelimishwa kuhusiana na masuala ya Sensa ya Watu na Makazi yam waka 2022 ili na wao wasaidie katika kutoa elimu kwa waumini wao na watu wanaowazunguka ambapo wameahidiwa kupatiwa elimu hiyo ili waendelea kusaidia kama walivyosaidia kwenye mazoezi mengine muhimu.

Kwa upande wao, Wakuu wa Wilaya wameshukuru kwa ushirikiano wanaoupata kutoka kwa viongozi wa dini na kuwaomba waendelee kutoa ushirikiano kwa viongozi wa serikali ili kuleta amani katika jamii.

Mkutano huo umehudhuriwa pia na Katibu Tawala wa Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Kamati ya Usalama ya Mkoa, Wakurugenzi wa Halmashauri, wakuu wa baadhi ya taasisi za Serikali.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.