• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Hapi atoa mwezi mmoja kukamilisha vyoo Sekondari ya Buturi

Posted on: July 16th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ametoa mwezi mmoja Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya akamilishe ujenzi wa choo katika Shule ya Sekondari ya Buturi iliyopo katika Mji wa Shirati.

Akizungumza katika mkutano wa wananchi katika Mji wa Shirati leo tarehe 15 Julai 2021 Mheshimiwa Hapi amepokea malalamiko kutoka kwa mwananchi kuhusu shida ya vyoo inayowakabili wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Buturi.

“Ninatoa mwezi mmoja hadi tarehe 15 Agosti 2021 choo cha Sekondari ya Buturi kiwe kimekamilika na kinahudumia wanafunzi wa shule hiyo” alisema Mheshimiwa Hapi.

Aidha Mheshimiwa Hapi ameagiza kuacha mara moja kutoza shilingi 2,000 kwa wafanyabiashara wa chakula kwa ajili ya fomu ya kupima afya na badala wake wafanyabiashara wapatiwe fomu hiyo wakatoe nakala.  

Mkuu wa Mkoa wa Mara alitoa maagizo hayo kufuatia Bwana Musa Mbogo kueleza kero ya choo katika Sekondari ya Katuru na jitihada ambazo wananchi walizifanya kunusuru hali hiyo.

Bwana Mbogo ameeleza kuwa baada ya wananchi kuona wanafunzi wa shule hiyo hawana choo walichangia kuchimba shimo, matofali na fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa choo hicho lakini fedha hizo kiongozi mmoja wa mtaa aliyehusika katika kuzikusanya amekimbia nazo.

Aidha Bwana Mbogo ameeleza kero nyingine kuwa ni zahanati ya eneo hilo ambayo ilikuwa inajengwa kwa nguvu za wananchi ambayo imesimama kwa muda mrefu bila taarifa za kueleweka.

Akitoa majibu ya kero hiyo Mtendaji wa Kata hiyo alieleza kuwa ni kweli wanachi walichangia nguvukazi, matofali na fedha kujenga choo na mhusika ametoroka na fedha hizo na kwa sasa kesi imelipotiwa polisi na mtuhumiwa bado anaendelea kutafutwa.

Aidha Mtendaji wa Kata alieleza kuwa kwa sasa walimueleza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Rorya ambaye aliahidi kutoa fedha kukamilisha ujenzi wa choo hicho.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya ameeleza kuwa alipewa taarifa na watendaji, alitenga shilingi milioni 3 ambazo zitakuja kukamilisha Chuo hicho.

Aidha katika mipango ya muda mrefu Halmashauri kwa kutumia bajeti ya 2021/2022 imetenga milioni 25 kutoka mradi wa P4R kwa ajili ya kujenga vyoo vingine katika Shule ya Sekondari ya Buturi.

Aidha Mkurugenzi aliahidi kufuatilia fedha shilingi 2,000 ambayo ilikuwa inatozwa na Afisa Afya kwa wafanyabiashara wa chakula kama ilikuwa inaingia kwenye mfuko wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya.

Katika mkutano na wananchi uliofanyika katika Mji wa Shirati, Mkuu wa Mkoa alitoa nafasi kwa wananchi kueleza kero zao na kuuliza maswali ambayo yalikuwa yanajibiwa na waatendaji mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya.

Mkuu wa Mkoa wa Mara alifanyaziara ya siku moja katika Wilaya ya Rorya na Tarime kukagua miradi ya Maji na mpaka wa Tanzania na Kenya katika wilaya hizo na aliongea na wananchi katika maeneo mbalimbali.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • RC atoa siku 14 wanafunzi wote Sekondari ya J. K. Nyerere wapate chakula shuleni

    July 28, 2025
  • Kusaya apokea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama

    July 25, 2025
  • Mtambi ataka matumizi ya GOTHOMIS kwa asilimia 100 Mara

    July 25, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.