• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Hapi ataka ubora katika utekelezaji wa afua za lishe Mara

Posted on: February 17th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi leo amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri kuchukua hatua za maksudi kuboresha utekelezaji wa afua za Lishe ili kuboresha lishe ya wananchi wa Mkoa wa Mara. 

Mheshimiwa Hapi ametoa maagizo hayo wakati wa kikao cha tathmini ya masuala ya lishe kilichofanyika leo katika ukumbi wa Uwekezaji uliopo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

“Haiwezekani kadi alama ya lishe kwa kipindi cha nusu mwaka bado inaonyesha Mkoa wa Mara tupo kwenye alama nyekundu katika kutoa fedha na katika kuweka katika bajeti fedha inayohitajika kwa kila mtoto wa chini ya umri wa miaka mitano” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuwachukulia hatua Maafisa Lishe na watendaji wengine wote wanaokwamisha utekelezaji wa afua za lishe katika Mkoa wa Mara.

“Kila mtu awasimamie watu wa eneo lake na wakichukuliwa hatua ushahidi ubaki katika mafaili yao ili kuhakikisha kuwa kazi zinafanyika kwa ufanisi, weredi na uzalendo” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ameagiza vikao vya tathmini ya masuala ya lishe kufanyika katika ngazi za Halmashauri na Wilaya mwishoni mwa mwezi Machi, 2022 ili mapungufu yanayoonekana yafanyiwe kazi kabla ya kuletwa katika kikao cha tathmini ya lishe kwa ngazi ya Mkoa.

Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuangalia uwezekano wa kuingiza fedha za miradi ya wadau wa maendeleo katika bajeti zake ili ziweze kutumika pamoja na mambo mengine kutekeleza masuala ya afua za lishe.

Awali, taarifa ya utekelezaji wa afua za lishe, Halmashauri zote za Mkoa wa Mara kwa kipindi cha kuanzia Julai, 2021 hadi Desemba, 2021 zilitenga fedha chini ya asilimia 50 inayohitajika lakini hata kiasi hicho cha fedha kilichotengwa pia kilitumika kwa kiasi kidogo au hakikutumika kabisa katika kipindi hicho. 

Aidha, katika taarifa hiyo, Halmashauri nne hazikutenga pesa wala hazikutumia pesa kabisa katika kipindi hicho cha tathmini, Halmashauri hizo ni Halmashauri ya Wilaya ya Butiama, Mnispaa ya Musoma, Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti na Halmashauri ya Wilaya ya Tarime.

Wakitoa maelezo kuhusiana na hali hiyo, wakurugenzi wa Halmashauri zote wamekiri kutenga na kutumia fedha ambazo zilitokana na wadau wa maendeleo na fedha za mapato ya ndani lakini hazikuonekana kwenye mfumo wa lishe kutokana na kuwa hazikuingizwa kwenye bajeti ya Halmashauri au zilitumika baada ya tarehe 15 Desemba, 2021 na hivyo kutoonekana katika tathmini ya wakati huu badala yake  zitaonekana katika kipindi kijacho cha tathmini.

 Kikao cha tathmini ya afua za lishe katika Mkoa wa Mara kimehudhuliwa na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa Bwana Benjamini Oganga, Wakuu wa Wilaya, Mganga Mkuu wa Mkoa, Wakuu wa Idara za Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Wakurugenzi wa Halmashauri, Waganga Wakuu wa Halmashauri na Maafisa Lishe wa Halmashauri zote za Mkoa wa Mara

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • RC atoa siku 14 wanafunzi wote Sekondari ya J. K. Nyerere wapate chakula shuleni

    July 28, 2025
  • Kusaya apokea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama

    July 25, 2025
  • Mtambi ataka matumizi ya GOTHOMIS kwa asilimia 100 Mara

    July 25, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.