• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Hapi ataka mradi wa Mgango- Kiabakari uwanufaishe wanamara

Posted on: July 25th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi amemuagiza mkandarasi wa mradi wa maji wa Mgango-Kiabakari kuhakikisha anaajiri vibarua katika ujenzi wa mradi huo kutokana na wananchi wa Mkoa wa Mara na kununua baadhi ya vifaa ya ujenzi huo kwa wafanyabiashara wa Mkoa wa Mara ili kuleta maendeleo ya Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Hapi ametoa maagizo hayo leo tarehe 19 Julai 2021 wakati akikagua mradi wa maji wa Mgango- Kiabakari na kujionea ujenzi wa miundombinu kwa ajili ya upanuzi wa mradi huounaosambaza maji katika sehemu kubwa ya vijiji vya Wilaya ya Butiama.

“Tunataka fedha ya mradi huu inawanufaishe wananchi wa Mkoa wa Mara na baadaye hawa ndio watakaotusaidia katika ulinzi wa miundombinu ya mradi huu” alisema mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi amemuagiza mkandarasi kuongeza kasi ya ujenzi wa mradi huo hususan eneo linapojengwa miundombinu ya kuchuja maji jirani na chanzo cha maji kwani mvua zikianza kazi haitaweza kuendelea.

“Hapa ninataka kazi ifanyike usiku na mchana na vibarua waongezwe ili kasi ya ujenzi iongezeke, mvua zikianza zikute mradi huu umeshakaa sawa na uweze kuendelea hata kipindi cha mvua” alisema Mheshimiwa Hapi.

Aidha amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji ya Mgango- Kiabakari kufanya mchakato wa haraka kununua pampu na kumtafuta mkandarasi wa kuifunga pampu hiyo ili huduma ya maji iweze kurejea katika wilaya ya Butiama kufuatia kuungua kwa pampu iliyokuwa inasukuma maji katika mradi wa zamani.

Aidha amewataka wananchi wanaotegemea maji kutoka katika Mamlaka ya Mgango- Kiabakari kuwa na subira katika kipindi hiki ambapo mchakato wa kununua pampu mpya unaendelea ili kuweza kufuata sheria za manunuzi.

Awali akitoa taarifa ya Mradi huo, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maji ya Mgango- Kiabakari Mhandishi Cosmas Sanda ameeleza kuwa Mamlaka hiyo kwa sasa inamiradi miwili mradi mpya ulioanza kujengwa na mradi wa wazamani na yote haitoi maji kwa wananchi.

“Mradi wa zamani hautoi maji kwa sababu pampu ya kusukuma maji imekufa lakini tayari serikali imetoa fedha na mchakato wa manunuzi ya kununua pampu na mtaalamu wa kufunga pampu hiyo unaendelea, tunategemea wananchi wataanza kupata maji baada ya miezi miwili” alisema Mhandisi Sanda.

Aidha Mhandisi Sanda ameeleza kuwa mradi wa pili ujenzi wake mkandarasi wake alipatikana tarehe 17 Desemba 2020 na mradi ulianza kujengwa Machi 2021 baada ya Government Notice kutolewa na mradi huo unategemewa kutekelezwa kwa miezi nane kwa gharama ya shilingi bilioni 70.78.

 “Kwa sasa mradi huu mpya upo umekamilika kwa asilimia 14 jumla katika kazi zinazohusisha ujenzi wa matanki ya maji, kusambaza mabomba, kukarabati baadhi ya matanki ya mradi wa zamani, kujenga nyumba ya watumishi na chujio la kusafishia maji na nyumba ya mtumishi” alisema Mhandisi Sanda.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.