• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

hapi aongoza kikao cha maandalizi ya Mara Day 2021

Posted on: August 6th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi leo tarehe 5 Agosti 2021 ameongoza kikao cha maandalizi ya Siku ya Mara inayotarajia kufanyika tarehe 15 Septemba 2021 katika Wilaya ya Tarime.

Akizungumza katika kikao hicho Mheshimiwa Hapi amewataka wadau wa utalii na mazingira kuchangia maandalizi ya siku hiyo ili iweze kufana na kuwahamasisha wadau waweze kushiriki.

“Niwaombe wadau wote waweze kushiriki katika kuchangia maandalizi ya Siku ya Mara sio tu kwa fedha lakini hata kwa mawazo ili maadhimisho haya yaweze kuboreshwa na kuwa mazuri zaidi” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ameiagiza kamati ya maandalizi ya Siku ya Mara kuitangaza siku hiyo kitaifa na kimataifa ili kuimarisha jina la Mkoa wa Mara kwa wadau wake wa ndani na nje ya nchi.

Mheshimiwa Hapi amewataka Wakuu wa Wilaya kufufua siku za usafi na vikundi vya kufanya mazoezi katika wilaya zao ili kuimarisha afya za wananchi wa Mkoa wa Mara.

Aidha katika kutengeneza jina la Mkoa wa Mara, Mheshimiwa Hapi amesimamisha mashindano yote ya mbio yanayoitwa Serengeti katika Mkoa wa Mara hadi hapo Mkoa utakapopata mbio ambazo zitakazoutambulisha mkoa kitaifa na kimataifa.

Maadhimisho ya Siku ya Mara ni ya kimataifa yenye lengo la kuhamasisha utunzaji wa mazingira yanayouzunguka Mto Mara ambao unaanzia katika milima ya Mai nchini Kenya na kumwaga maji yake katika Ziwa Victoria katika Mkoa wa Mara.

Maadhimisho ya Siku ya Mara yanafanyika kila mwaka katika nchi za Kenya na Tanzania yakihusisha wadau mbalimbali hususa wadau wa utalii, maji na mazingira.  

Wakati huo huo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Albert Gabriel Msovela ameeleza kuwa Mkoa wa Mara pia unaandaa Maonyesho ya Teknolojia ya Madini na Wajasiriamali yatakayofanyika Oktoba 2021 katika eneo la Bweri nyuma ya stendi kuu ya mabasi.

Bwana Msovela ameeleza kuwa maonyesho hayo yatahusisha wadau wa madini na ujasiriamali kutoka katika Mikoa yote ya Kanda ya Ziwa ambayo ni Mara, Simiyu, Mwanza, Shinyanga, Kagera na Geita.

“Mpaka sasa tumeshapata eneo la ekari 10.3 kwa ajili ya maonyesho hayo na lipo katika eneo la Bweri katika Manispaa ya Musoma” alisema Bwana Msovela.

Ameeleza kuwa awali kulikuwa na mpango wa kuandaa maonyesho ya madini na baadaye likaja wazo la kuunganisha na wajasiriamali wadogo ili kuyapa nguvu zaidi maonyesho hayo.

Kikao kingine cha maandalizi ya shughuli hizi kinategemewa kufanyika tena tarehe 17 Agosti, 2021 katika ukumbi wa Uwekezaji uliopo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.