• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Hapi aitaka MMG kutekeleza maagizo ya Serikali

Posted on: July 22nd, 2022

HAPI AITAKA MMG KUTEKELEZA MAAGIZO YA SERIKALI

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ameutaka Mgodi wa Dhahabu wa MMG Limited kutekeleza maagizo ya serikali yanayotolewa kwa mujibu wa sheria mbalimbali zinazosimamia sekta ya madini hapa nchini.

Mheshimiwa Hapi ametoa agizo hilo leo tarehe 19 Julai, 2022 wakati alipoutembelea mgodi huo uliopo katika Kijiji cha Seka, katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma na kuutaka kutoa maelezo ya kukiuka maagizo yake aliyotoa awali.

“Ninataka mgodi utoe maelezo kwa nini haujatekeleza maagizo yangu na maagizo ya ofisi ya madini Mkoa wa Mara kuhusu kulipa ushuru wa huduma, kuwa na mpango wa uwajibikaji kwa jamii (CSR) na kuwa na Meneja Mkuu wa Kampuni” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa ushuru wa huduma na CSR sio msaada, ni masuala ya kisheria lazima yatekelezwe na wawekezaji wote hapa nchini kwa ajili ya maendeleo ya Halmashauri hiyo.

Wakati huo huo, Mheshimiwa hapi ameuagiza mgodi huo kuandaa mpango wa kufunga mgodi huo kwa mujibu wa sheria na kuutaka mgodi huo kuwasilisha majina ya kampuni, thamani ya zabuni walizopewa na muda wa utekelezaji ili wazabuni hao waweze kulipa ushuru wa huduma na CSR kwa Halmashauri.

Mheshimiwa Hapi pia ameushauri mgodi huo kujenga uzio kuzunguka eneo lake ili kuzuia uhalifu unaoweza kujitokeza kwa kuwa hauna uzio katika sehemu kubwa ya mgodi huo.

Mheshimiwa Hapi ameutaka mgodi huo kumlipa Bibi Sharma Mwanyoka mjasiriamali ambaye alikuwa anafanya biashara na mgodi huo ambaye anadai shilingi milioni 5 kuanzia mwaka 2018.

Aidha, ameutaka mgodi huo kuajiri Afisa Uhusiano ili kuweka mahusiano mazuri na wananchi wanauzunguka mgodi huo na kuachana na mfumo wa sasa ambapo Meneja wa Utawala ndiye Mhasibu, mtu wa utawala na Afisa Uhusiano mtu mmoja.

Kwa upande wake, Afisa Madini Mkoa wa Mara Mhandisi Joseph Kumburu ameeleza kuwa katika ukaguzi wa wataalamu wa madini katika mgodi huo, waliagiza mgodi huo kumteua Meneja Mkuu ambaye kwa mujibu wa Sheria za Madini ndiye mtu wa kuzungumza na serikali.

“Kwa sasa, hawana mtu mwenye cheo hicho na kila wakiitwa kwa jambo fulani wanamleta afisa tofauti kwenda kusilikiliza na tuliwapa muda wa siku 30 zimeshaisha lakini suala hilo halijatekelezwa” alisema Mhandisi Kumburu.

Aidha, Mhandisi Kumburu ameeleza kuwa mgodi ulikuwa umeelekezwa kununua mavazi zaidi ya usalama (PPE) kwa ajili ya wafanyakazi lakini hawajatekeleza.

Bwana Kumburu ameeleza kuwa mgodi huo uliagiza pia kumwaga maji katika barabara zake ili kupunguza vumbi kwa wananchi wanaouzunguka mgodi huo ambalo halijatekelezwa.

  Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Katibu Tawala wa Mkoa, kamati ya usalama ya Mkoa, Wilaya ya Musoma na baadhi ya watumishi kutoka ofisi ya madini, ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.