• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Hapi aishukuru Benki NMB kwa msaada

Posted on: July 16th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ameipongeza Benki ya NMB kwa msaada mkubwa uliyoitoa katika sekta za elimu na afya katika Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Hapi ametoa pongezi hizo wakati wa hafla fupi ya kupokea msaada huo iliyofanyika katika Shule ya Msingi Buhare iliyopo katika Manispaa ya Musoma leo tarehe 16 Julai 2021.

“Nimetaarifiwa kuwa NMB wametoa msaada wa vitanda, madawati, mabati na vifaa vya hospitali wenye jumla ya shilingi 140,000 katika Mkoa wa Mara, asanteni sana” amesema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa msaada uliotolewa katika Mkoa wa Mara ni mabati 2,580, madawati 937, vitanda nane kwa ajili ya Hospitali ya Rufaa Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere ambavyo vimegawiwa katika wilaya zote za Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa msaada uliotolewa na Benki ya NMB katika hafla hiyo ni sehemu ya msaada kubwa ambao wameutoa katika wilaya mbalimbali za Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa msaada huu unaendana na malengo ya Mkoa wa Mara na Serikali ya Awamu ya Sita kwa ujumla ya kuboresha huduma za jamii kwa wananchi wa Tanzania na hususan sekta za afya na elimu.

Aidha ameiomba Benki ya NMB kuendelea kutoa misaada ya hali na mali pale inapohitajika ili kuinua maendeleo ya Mkoa wa Mara.

Kwa upande wake, Mkuu wa Fedha wa Benki ya NMB Bwana Baraka Wenslaus ameeleza kuwa msaada uliotolewa ni sehemu ya fedha zaidi ya shilingi bilioni 2 ambazo zimetengwa na benki hiyo kama asilimia moja ya faida yake ya mwaka jana kwa ajili ya kuirudisha kwenye jamii.

“Mwaka jana Benki ya NMB ilipata faida ya shilingi bilioni 205 ambazo kwa mujibu wa sera za benki hiyo asilimia moja hurudishwa kwa jamii katika maeneo ya elimu, afya na elimu ya fedha na ujasiriamali kwa watanzania” ameeleza Bwana Wenslaus.

Ameeleza kuwa kwa Mkoa wa Mara wanamatumaini msaada walioutoa utaleta mabadiliko chanya na kuimarisha huduma za jamii katika sekta ya elimu na afya.

Katika hafla hiyo ya kupokea msaada, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Musoma Dkt. Alfany Haule, Afisa Elimu wa Mkoa wa Mara, Meya na Mkurugenzi wa Manispaa ya Musoma, Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara, viongozi wa CCM, walimu na wanafunzi.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.