• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Dkt. Nchimbi apewa kifimbo na familia ya Baba wa Taifa

Posted on: April 24th, 2025

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi leo ameendelea na ziara yake katika Wilaya ya Butiama ambapo ametembelea nyumbani kwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na kupewa kifimbo cha uongozi na familia ya Baba wa Taifa.  

Mhe. Nchimbi akiwa katika eneo hilo amepokelewa na kiongozi wa kabila la Wazanaki Chifu Josephat Wanzagi na mtoto wa Mwalimu Nyerere Ndugu Madaraka Nyerere na wanafamilia wengine.

Dkt. Nchimbi ameishukuru familia ya Baba wa Taifa kwa mapokezi mazuri aliyoyapata na akashukuru kwa zawadi ya fimbo na kuwaahidi kuyaenzi mazuri yote ambayo Baba wa Taifa aliyasimamia katika uhai wake.

Akizungumza wakati wa kukabidhi fimbo hiyo, Chifu Wanzagi amesema kifimbo hicho ni moja ya kifaa cha kazi atakachokitumia katika dhamana aliyopewa ya kuwatumikia Watanzania. na kuwataka watanzania kumuenzi Mwalimu Nyerere kwa vitendo.

“Fimbo hii huwa tunamkabidhi kiongozi tunayemkubali, tunayeona anafaa kuwatumikia Watanzania na kwa kuwa tumeona unazo sifa hizo ndio maana tumekukabidhi” amesema Chifu Wanzagi.

Akiwa Mwitongo, Dkt. Nchimbi ametembelea kaburi la Baba wa Taifa na kuweka shada, kuwasha mshumaa, kufanya sala fupi katika kaburi hilo na kufanya mazungumzo na familia ya Mwalimu Nyerere.

Balozi Nchimbi ameambatana na Mwenza wake, Mama Jane Nchimbi pamoja na viongozi wengine wa Chama na Serikali ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 61 Muungano wa Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar.    

Kauli mbiu ya miaka 61 ya Muungano ni “Muungano wetu ni Dhamana, heshima na tunu ya Taifa, Shiriki Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025”. 

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Zingatieni miongozo ya kilimo cha tumbaku- Dkt. Haule

    June 18, 2025
  • Mtambi aipongeza Bunda TC kwa hati safi miaka mitano mfululizo

    June 13, 2025
  • Mtambi aitaka Bunda DC kuwasilisha Mkakati wa kukusanya milioni 700

    June 13, 2025
  • Mtambi aipongeza Halmashauri ya Rorya

    June 12, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.