• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Bunda yatoa mapendekezo ya Mgawanyo wa Halmashauri

Posted on: April 28th, 2020

Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mwalimu Lyidia Bupilipili ameiomba Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMESEMI) inapogawa upya halmashauri za Wilaya ya Bunda kuzingatia suala la upatikanaji wa huduma kiurahisi kwa wananchi.

Mheshimiwa Bupilipili ameeleza hayo leo tarehe 22 Aprili wakati wa ziara ya Katibu Mkuu TAMISEMI Eng. Nyamhanga katika Wilaya ya Bunda.

“Ofisi yangu inapendekeza kuwa Halmashauri ya Mji wa Bunda iwe na Tarafa mbili za Serengeti na Chamliho na Halmashauri ya Wilaya ya Bunda iwe na tarafa mbili za Kenkombyo na Nansimo ili kuwarahisishia wananchi kupata huduma” alisema Mwalimu Bupilipili.

Ameeleza kuwa kwa sasa Wilaya hiyo ina tarafa nne ambapo Halmashauri ya Mji wa Bunda ina tarafa moja wakati Halmashauri ya Wilaya ya Bunda ina tarafa tatu ambapo mbili zipo upande mmoja wakati nyingine ipo upande mwingine wa wilaya na hivyo kuwalazimisha wananchi kuvuka mji wa Bunda ili kwenda kupata huduma ilipohamia Halmashauri ya Wilaya upande mwingine ambako ni mbali.

Mheshimiwa Bupilipili ameeleza kuwa ofisi yake imependekeza kuwa ofisi za makao makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Bunda yajengwe Kibara kama ilivyopendekezwa na Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo na mapendekezo hayo tayari yamewasilishwa TAMISEMI.

Awali, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda Mwalimu Amos J. Kusaja alisema Halmashauri ilipokea agizo la kuhamishia ofisi zake kwenye maeneo yao ya utawala na Baraza la Madiwani waliamua kuhamishia ofisi katika mji wa Kibara ambako wako hadi sasa.

Bwana Kusaja alisema Baraza la Madiwani liliamua Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ijengwe katika Tarafa ya Chamliho na Menejimenti ya Halmashauri ilipendekeza kuwa kutokana na hilo, ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Bunda zijengwe katika kijiji cha Makongoro jirani na hospitali ya wilaya mapendekezo ambayo hayakupitishwa na Baraza la Madiwani.

“Baada ya maamuzi ya madiwani, sisi katika menejimenti hatuna tena suala lingine tunasubiria maamuzi ya TAMISEMI na viongozi wengine” alisema Bwana Kusaja.

Kwa Upande wake Katibu Mkuu TAMISEMI, Mhandisi Joseph Nyamhanga amesema TAMISEMI hufanya maamuzi yake kutegemea mapendekezo yaliyopokelewa na hususan maamuzi ya Baraza la Madiwani ambayo ni ya kisheria.

“Yaleteni tena mapendekezo hayo tuyaangalie vizuri, ili yaweze kufanyiwa kazi mara moja” alisema Eng. Nyamhanga.

 Katibu Mkuu TAMISEMI alikuwa na ziara ya siku tatu katika Wilaya ya Tarime, Serengeti na Bunda katika Mkoa wa Mara kuanzia tarehe 20 Aprili 2020 hadi tarehe 22 Aprili 2020.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.