• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Wananchi waaswa kuacha kulima kwenye vyanzo vya maji

Posted on: June 28th, 2022

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Bwana Sahili Nyanzabara Geraruma amewataka wananchi wa Kata ya Itiriyo iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime kuacha kulima katika chanzo cha maji ili mradi wa maji uliojengwa katika eneo hilo uweze kuleta matokeo yanayotarajiwa.

Bwana Geraruma ametoa agizo hilo leo akiwa katika eneo la Itiriyo kabla ya kuweka jiwe la msingi katika mradi wa maji wa Itiriyo.

“Ninawaasa wananchi wanaolima karibu na chanzo cha maji cha mradi huu kuacha kabisa kulima eneo hilo kwa sababu chanzo kile kinatokana na chemichemi ambayo inaweza kukauka au kutoa maji kidogo kama chanzo hicho hakitatunzwa vizuri” alisema Bwana Geraruma.

Aidha Bwana Geraruma katika maeneo mbalimbali amewakumbusha wananchi kushiriki sensa ya watu na makazi na kuachana na biashara na matumizi ya dawa za kulevya.  

Bwana Geraruma amewataka viongozi wa Wilaya ya Tarime kuhakikisha wananchi wanaacha kulima mara moja katika eneo hilo ili kulinda chanzo cha maji cha mradi wa maji wa Itiriyo.

Aidha Bwana Geraruma ameitaka Wakala wa Maji Vijijini (RUWASA) kuweka uzio katika eneo la chanzo na eneo lilipo tenki la maji na pampu yam aji ili kulinda miundombinu na vifaa vilivyopo katika maeneo hayo.

Wakati huo huo, mbio za Mwenge wa Uhuru zimeendelea leo katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime ambapo ukiwa katika Halmashauri hiyo umeweka mawe ya msingi, kuzindua na kukagua miradi yote iliyokuwa imepangwa.

Miradi iliyowekewa mawe ya msingi ni pamoja na mradi wa maji Itiriyo, daraja la kebweye, Kituo cha Afya cha Bumera, na Shule mpya ya Sekondari Kata ya Sirari na umezindua Klabu ya Wapinga Rushwa katika Shule ya Sekondari ya Nyamwigura.  

Aidha Mwenge wa Uhuru pia ukiwa katika Halmashauri hiyo umeteketeza madawa ya kulevya katika eneo la Turugeti-Runyerere na katika eneo la mkesha, Mwenge umekagua vikundi vya wanawake, vijana, walemavu, banda la Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) na shughuli za uhamasishaji wa wananchi kushiriki sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022.

Katika kuupokea Mwenge wa Uhuru, wananchi wengi sana walijitokeza na kubeba matawi ya miti kushangilia Mwenge wa Uhuru kuanzia eneo la makabidhiano hadi eneo la mkesha.

Mwenge wa Uhuru kesho tarehe 29 Juni, 2022 utaendelea na mbio zake katika Halmashauri ya Mji wa Tarime.  

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa