• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

Posted on: August 1st, 2025

Adeladius Makwega-Musoma MARA.

Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kanali Evans Alfred Mtambi leo Agosti Mosi, amempokea na kuzungumza na Prof. Charles Lukiko Majige na kuzungumzaia umuhimu wa wananchi wa Mkoa wa Mara kulima zao la alizeti kutokana na kuwa na faida nyingi kwa wakulima.

“Natambua kuwa kilimo cha zao la alizeti kinatupatia mafuta ya kula, vyakula vya mifugo lakini pia kilimo cha alizeti kinasaidia kuzuia tembo kufanya uharibifu jirani na makazi ya binadamu” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amempongeza Prof. Majige ambaye baada ya kustaafu ameamua kuwekeza kwa kujenga kiwanda cha mafuta ya alizeti na kulima katika eneo la Majita, Halmashauri ya Wilaya ya Musoma na kuwataka wananchi kuwaunga mkono wawekezaji wanaowekeza katika maeneo yao.

“Baadhi ya maeneo yetu, mtu akienda kuwekeza, madai yanakuwa huyu ni mtia, siyo kila anayewekeza ni mtia nia, watu wengi wanataka kuzikomboa jamii zao walipozaliwa sio kwa sababu za kisiasa” amesema Mhe. Mtambi.

Kanali Mtambi aamesema kuwa Mkoa wa Mara una wanyama pori wengi hususan katika maeneo yanayopakana na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na mapori ya akiba ya Ikorongo na Guremeti ambapo amesema tembo katika maeneo hayo wanaweza kudhibitiwa kwa kilimo cha Alizeti.

Mhe. Mtambi ameahidi Prof. Majige kuwa atashiriki kama mgeni rasmi katika tamasha la Kiutamaduni la kabila la Wajita litakalofanyika katika eneo la Bukima tarehe 15 Agosti, 2025 litakalohusisha ngoma, michezo, nyimbo na vyakula na matunda ya kiutamaduni wa kabila la Wajita.

Mhe. Mtambi amempongeza Prof. Majige kwa kuandaa tamasha hilo na kuongeza kuwa tamasha hilo ni uhimu katika kuifundisha jamii tamaduni na mambo mazuri yaliyokuwepo zamani ambayo kwa sasa yanapotea.

Aidha, Kanali Mtambi amemshukuru Prof. Majige kwa zawadi ya mafuta ya kula aliyompatia yaliyozalishwa katika kiwanda chake alichokianzisha.  

Mhe. Mtambi amemuagiza Afisa Kilimo kutoka Sekretarieti ya Mkuu wa Mkoa wa Mara kufuatilia upatikanaji wa mbegu za alizeti za ruzuku kwa wakulima kama sehemu ya kuwahamasisha kulima zao hilo ili kujiimarisha kiuchumi.

Kwa upande wake, Prof. Majige amesema amefungua kiwanda cha mafuta ya alizeti ili kuwahamasisha wananchi wa Mkoa wa Mara kulima alizeti kama zao la biashara na kuwaletea soko la uhakika la alizeti yao kupitia kiwanda hicho.

Prof. Majige amesema kuwa kiwanda hicho ambacho kipo katika eneo la Saragana kinauwezo mkubwa wa kuzalisha mafuta lakini kina changamoto ya kupata alizeti ya kutosha ili kiwanda hicho kiweze kufanyakazi kwa ufanisi.

Prof. Majige ambaye pia ni Chifu wa Wajita amesema kutokana na aina ya udongo uliopo, wananchi wakihamasishwa kulima kama zao la biashara, kilimo cha alizeti kinaweza kuwanyanyua kiuchumi kutokana na mahitaji ya alizeti katika viwanda vya ndani na nje ya Mkoa wa Mara.  

 Katika mazungumzo hayo Mkuu wa Mkoa alikuwa amewakaribisha maafisa mbalimbali kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa