• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Wananchi wa Nyatwali waanza kupokea fidia

Posted on: September 10th, 2024

Zaidi ya wananchi 3,500 wa Kata ya Nyatwali, Wilaya ya Bunda wanaohama kupisha eneo la ushoroba wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti (SENAPA) leo tarehe 9 Septemba, 2024 wameanza kulipwa fidia zao zoezi lililoongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mhe. Dkt. Vincent Naano Anney.

Akizungumza wakati wa kuanza kwa utoaji wa malipo ya fidia Dkt. Anney amemshukuru Rais kwa kuamua kulipa fidia za wananchi mapema ili waweze kuendelea na shughuli zao za maendeleo katika sehemu nyingine.

“Jambo hili lilichukua muda mrefu lakini sasa limefikia mwisho wake, niwaombe wananchi mkishachukua fidia muanze kufanya shughuli za maendeleo katika maeneo mapya ili kuzitumia fedha hizi kabla ya kuzitumia katika mambo yasiyo na msingi” amesema Mhe. Anney.

Aidha, amezitaka familia zenye migogoro kuhusu umiliki wa ardhi katika eneo hilo kumaliza migogoro hiyo haraka ili waweze kulipwa fidia zao na kuendelea na maisha mengine.

Kwa upande wake, Kamishna wa Uhifadhi wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Bwana Mussa Kuji ameishukuru Serikali kwa kutoa fedha za kuwafidia wananchi wa Kata ya Nyatwali na kuwapongeza wananchi kwa kukubali kufidiwa ili kupisha shughuli za uhifadhi katika eneo hilo.

“Tuko kwenye zoezi muhimu sana, nimefurahi kuona wananchi wako tayari kufidiwa na kuruhusu kuachia eneo hili ili kutumika katika shughuli za uhifadhi” amesema Bwana Kuji.

Bwana kuji amewapongeza wananchi kwa kuonyesha umoja na mshikamano na kuongeza kuwa wananchi wengi alioongea nao wamefurahia kulipwa fidia na kwenda sehemu nyingine yenye amani na utulivu na kuondokana na usumbufu wa wanyama wakali katika makazi yao.   

Bwana Kuji amesema kwa sasa ikolojia ya Serengeti imerudi nah ii itaongeza utalii kw aupande wa magharibi na inategemea kuongeza watalii milioni 5 na kuleta mapato ya dola za kimarekani bilioni 6 ifikapo 2025.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa hundi ya malipo, Bi. Mgesi Kisuka Mchiro, Mkazi wa Mtaa wa Tamau ameishukuru Serikali kwa kutekeleza ahadi yake ya kutoa fidia na kwamba sasa familia yake itaondokana na adha ya wanyama wakali waliyokuwa wanaipata katika eneo hilo.

Kata ya Nyatwali ipo magharibi mwa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na wananchi wake wameanza kulipwa ili kupisha uhifadhi na uendelezaji wa eneo hilo ambalo ni mapito ya wanyama na hususan wakati wa kiangazi wanapoenda kunywa maji Ziwa Victoria pembezoni mwa Barabara ya Mwanza –Musoma.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa