• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Wadau toeni ushirikiano kwa TEMESA

Posted on: December 19th, 2023

Uongozi wa Mkoa wa Mara umeyataka taasisi na mashirika ya umma yaliyopo katika Mkoa wa Mara kutoa ushirikiano kwa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) ili waweze kutoa huduma bora na endelevu.

Akizungumza katika ufunguzi wa Mkutano wa Wadau wa TEMESA katika Mkoa wa Mara uliofanyika leo katika ukumbi wa Mwembeni Complex kwa Niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mhe. Dkt. Khalfan Haule amesema kuwa pamoja na Serikali kufanya maboresho makubwa katika utendaji wa TEMESA, wadau wasipotoa ushirikiano na huduma haziwezi kuimarika.

“Taasisi zote zikilipa madeni yake wanayodaiwa na TEMESA kwa wakati, TEMESA itaweza kuwalipa wazabuni wake na kuimarisha utendaji wake na hivyo taasisi nazo zitapata huduma bora zinazotegemewa” amesema Dkt. Haule.

Mhe. Haule ameipongeza TEMESA kwa  kuchukua hatua ya kujifanyia tathmini kwanza kabla ya kukutana na wadau ili kuwapa nafasi na wao kutoa maoni yao kuhusu shughuli zinazofaywa na wakala huyo katika maeneo yao ili waweze kuboresha.

Aidha, Mhe. Haule ameipongeza TEMESA kwa kuamua kufanya mabadiliko chanya katika utendaji wao na hususan kwa kuwekeza katika vifaa na rasilimali watu ili kuboresha huduma wanazozitoa kwa taasisi mbalimbali za Serikali hapa nchini.

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa TEMESA Bwana Lazaro Kilahala ameeleza kuwa TEMESA ilianza kufanyakazi mwaka 1925 kama Idara ndani ya Wizara inayohusika na Ujenzi na baadaye kuanzishwa Wakala unaojitegemea mwaka 2006.

“Kwa sasa tumeamua kama Wakala kubadilika, na kutokana na mabadiliko hayo tumeanza kuwekeana makubaliano ya kimkataba na taasisi mbalimbali za Serikali kutoa huduma za matengenezo ya magari ikiwa ni pamoja na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na taasisi nyingine” amesema Bwana Kilahala.

Bwana Kilahala pia ameeleza kuwa kwa sasa Wakala inanunua vilainishi na vifaa vya umeme moja kwa moja kutoka kwa wazalishaji ili kupunguza gharama na kudhibiti ubora wa vifaa wanavyotumia katika matengenezo.

Bwana Kilahala ameeleza kuwa kwa sasa Wakala hiyo inzo karakana 27 na vivuko na inafanya shughuli zake kwa kusaidiana na watoa huduma walioainishwa katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Ameyataja majukumu ya TEMESA kuwa ni kufanya matengenezo ya magari, pikipiki na mitambo ya Serikali; kufanya matengenezo na usimikaji wa mifumo ya umeme, mabarafu, viyoyozi, na Elekroniki inayomilikiwa na Serikali; na uendeshaji na usimamizi wa vivuko vya Serikali. 

 Ameyataja majukumu mengine kuwa ni kutoa ushauri wa kitaalamu kwa Serikali na Umma kwa ujumla katika nyanja za uhandisi wa mitambo, umeme, na elekroniki; na kukodisha mitambo mbalimbali kama vile mitambo ya kuzalisha kokoto na mitambo ya kazi za barabara.

 Kikao hiki kimehudhuriwa na Wakuu wa Wilaya, Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mara, Wakuu wa Idara na Vitendo, Wakurugenzi wa Serikali za Mitaa, taasisi na mashirika ya umma, wazabuni  na wadau wengine wa TEMESA, Menejimenti na watumishi wa TEMESA. 

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mtambi aipongeza Bunda TC kwa hati safi miaka mitano mfululizo

    June 13, 2025
  • Mtambi aitaka Bunda DC kuwasilisha Mkakati wa kukusanya milioni 700

    June 13, 2025
  • Mtambi aipongeza Halmashauri ya Rorya

    June 12, 2025
  • Mtambi awataka wanawake kugombea nafasi za uongozi

    June 12, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa