• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Ufaulu wa Darasa la Saba wapanda Mara

Posted on: November 25th, 2023

Ufaulu wa Mtihani wa Taifa wa Kumaliza Shule ya Msingi (PSLE) katika Mkoa wa Mara kwa mwaka 2023 umepanda ambapo jumla ya watahiniwa 52,731 sawa na asilimia 75 ya watahiniwa wote 70,182 waliofanya mtihani huo wamefaulu kwa kupata madaraja A, B na C.

Taarifa iliyotolewa na Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu Bwana Makwasa Bulenga imeeleza kuwa kati ya wanafunzi waliofaulu mtihani huo kwa mwaka 2023 wavulana ni 26,438 na wasichana ni 26,288.

Bwana Makwasa ameeleza kuwa mwaka 2022 Mkoa wa Mara ulikuwa na watahiniwa waliofaulu walikuwa 57,393 sawa na asilimia 74.53 ya wanafunzi wote waliofanya mtihani, ukilinganisha na mwaka huu ufaulu wa mwaka huu umepanda kwa asilimia 0.47.  

“Wanafunzi wote walioanza darasa la kwanza mwaka 2017 walikuwa 90,300 ambapo kati yao wavulana walikuwa 44,900 na wasichana walikuwa 45,406 hata hivyo wanafunzi waliofanya mtihani huo walikuwa 70,182” amesema Bwana Bulenga.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa jumla ya watahiniwa 3,258 ambao ni sawa na asilimia 5.96 waliokuwa wameandikishwa kufanya mtihani katika Mkoa wa Mara hawakufanya kutokana na sababu mbalimbali.

Taarifa ya Bwana Bulenga imeitaja Halmashauri iliyofanya vizuri katika mtihani huo kuwa ni Manispaa ya Musoma, ikifuatiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Rorya, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, Halmashauri ya Wilaya ya Bunda na Halmashauri ya Mji wa Bunda.

Halmshauri nyingine ni Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, Halmashauri ya Wilaya ya Butiama, Halmashauri ya Mji wa Bunda na ya mwisho ni Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti.  

Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi umefanyika hapa nchini tarehe 13-14 Septemba, 2023 na matokeo yake kutolewa na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) tarehe 25 Novemba, 2023.

Wakati huo huo, Baraza la Mtihani la Tanzania limefungia vituo vya mtihani viwili (02) kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti Mkoa wa Mara vilivyothibitika kupanga kufanya udanganyifu katika mtihani huo mpaka hapo Baraza litakapojiridhisha kuwa ni salama kwa uendeshaji wa Mitihani ya Taifa.

Taarifa ya Baraza la Mitihani kuhusu matokeo ya mtihani wa Darasa la Saba,2023 imeeleza kuwa  Baraza limechukua hatua hiyo kwa mujibu wa Sheria za Mitihani na kifungu 4 (8) cha Kanuni za Mitihani za Mwaka 2016.  

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa