• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TMDA yatoa msaada wa dawa Magereza Mara

Posted on: June 24th, 2022

Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Kanda ya Ziwa Mashariki leo imekabidhi dawa zenye thamani ya shilingi 23,000,000 kwa Mwakilishi Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara kwa ajili ya Magereza za Mkoa wa Mara.

Akikabidhi dawa hizo, Meneja wa TMDA Kanda ya Ziwa Mashariki Bi. Sophia Mziray ameeleza kuwa msaada huo wa dawa ni kwa ajili ya magereza zote za Mkoa wa Mara.

“Tunatambua kuwa kuna upungufu wa dawa katika magereza za Mkoa wa Mara, msaada huo utazisaidia magereza kuweza kutoa huduma kwa wafungwa na watu wengine wanaohudumiwa kiurahisi zaidi” alisema Bi. Mziray

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara ambaye pia ni Kaimu Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Afya Dkt. Juma Mfanga ameishukuru TMDA kwa msaada huo na kuitaka kuendelea kutoa msaada katika Mkoa wa Mara.

“Kuna upungufu wa dawa kwenye magereza zetu, kwa msaada huu tuliopokea leo zinaweza kuwasaidia walengwa wa dawa hizi” alisema Dkt. Mfanga.

Aidha Dkt. Mfanga ameitaka Jeshi la Magereza Mkoa wa Mara kutumia dawa hizo kulingana na matumizi yaliyokusudiwa.

Kwa upande wake, Kamanda wa Magereza Mkoa wa Mara Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Hospitus Mendi ameeleza kuwa TDMA Kanda ya Ziwa  Mashariki ni wadau wao wakubwa na mara kwa mara wanakuja kutoa mafunzo mbalimbali katika magereza yaliyopo katika Mkoa wa Mara.

“Mara ya mwisho walitoa elimu katika magereza ya Mkoa wa Mara kuhusiana na namna  ya kudhibiti ugonjwa wa Kifua Kikuu” alisema ACP Mendi.

Bwana Mendi ameeleza kuwa kwa dawa za kutumia katika magereza wanazipata zaidi kutoka kwa Kamishana wa Magereza nchini lakini kuna wakati hazitoshelezi mahitaji yao ya dawa.

Kamishna huyo Msaidizi ameeleza kuwa dawa hizo zilizotolewa msaada zitagawiwa katika magereza zote za Mkoa wa Mara ili ziweze kutumika kwa maksudi yaliyokusudiwa.

TMDA Kanda ya Mashariki inahudumia mikoa mitatu ambayo ni Mwanza, Simiyu na Mara na ofisi yake ipo katika eneo la Buzuruga, katika jiji la Mwanza.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mtambi aipongeza Bunda TC kwa hati safi miaka mitano mfululizo

    June 13, 2025
  • Mtambi aitaka Bunda DC kuwasilisha Mkakati wa kukusanya milioni 700

    June 13, 2025
  • Mtambi aipongeza Halmashauri ya Rorya

    June 12, 2025
  • Mtambi awataka wanawake kugombea nafasi za uongozi

    June 12, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa