• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TAMISEMI yapongeza vyumba vya VIP Hospitali ya Manispaa ya Musoma

Posted on: April 8th, 2024

Mkurugenzi wa Idara ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii kutoka Ofisi ya Rais- TAMISEMI Dkt. Rashid Mfaume amefanya ziara ya kukagua ukarabati wa Hospitali ya Manispaa ya Musoma na kupongeza uanzishwaji wa wodi za wagonjwa wa VIP katika hospitali hiyo.

Dkt. Mfaume ametoa pongezi hizo baada ya kukagua wodi hizo na kuitaka Manispaa ya Musoma kufunga  televisheni katika wodi hizo na kuboresha huduma kwa wagonjwa watakaolazwa katika wodi hizo ili kuwavutia wengi zaidi kukaa kwenye wodi hizo na kuongeza mapato ya hospitali.

“Ubunifu huu ni jambo la kuigwa na Hospitali zote za Halmashauri hapa nchini ili katika ngazi ya msingi pawepo na huduma nzuri kwa viongozi na watu wenye uwezo wa kulipia ili kuongeza mapato ya hospitali na kutoa huduma bora kwa wananchi” amesema Dkt. Mfaume.

Dkt. Mfaume ameitaka Manispaa ya Musoma ukarabati utakapokuwa umekamilika kuitangaza huduma zitakazokuwa zinatolewa hapo ikiwa ni pamoja na kuonyesha vyumba hivyo pamoja na gharama zake ili wananchi waweze kutambua mabadiliko makubwa yaliyofanyika katika hospitali hiyo.

Aidha, Dkt. Mfaume amepongeza ukarabati mkubwa pamoja na ujenzi wa fensi uliofanyika katika hospitali hiyo baada ya Manispaa ya Musoma kukabidhiwa majengo ya iliyokuwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara mwezi Julai, 2023 baada ya hospitali hiyo kuhamia katika majengo jengo lao lililopo eneo la Kwangwa, Manispaa ya Musoma.

Dkt. Mfaume akiwa katika eneo hilo pia, alikagua ujenzi wa majengo mapya ya wagonjwa wa dharura, kinywa na meno na macho katika hospitali hiyo ambayo ujenzi wake uko katika hatua ya boma na kuitaka Manispaa ya Musoma kuongeza kasi ya ujenzi ili wananchi waweze kupata huduma mapema.

Hata hivyo, Dkt. Mfaume ameitaka Manispaa ya Musoma kuweka mchanganuo wa ukarabati kuonyesha kila jengo limetumia shilingi ngapi na kukarabati vitanda na samani nyingine ili ziweze kutumika kutoa huduma.

Aidha, ameipongeza Manispaa ya Musoma kwa kutoa mafunzo na matumizi ya mfumo wa GoTHOMIS ulioboreshwa kwa watumishi wa vituo vyote vya kutolea huduma za afya katika Manispaa hiyo na kuitaka Manispaa kufuatilia kibali cha kubadili matumizi ya sehemu ya fedha za ukarabati ili kujenga duka la dawa la hospitali.

Akitoa taarifa ya ukarabati huo, Mkuu wa Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe wa Manispaa ya Musoma Dkt. Mustafa Waziri amesema Manispaa ilipokea jumla ya shilingi bilioni 1.3 ambapo milioni 500 zilikuwa kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa fensi na milioni 800 zilikuwa kwa ajili ya ujenzi wa majengo mapya.

Dkt. Mustafa ameeleza kuwa hadi sasa ukarabati na ujenzi wa fensi umekamilika na fedha iliyobakia katika mradi huo imetumika kujenga duka la dawa la hospitali hiyo kwa gharama ya shilingi milioni 39 huku ujenzi wa majengo mapya unaendelea.

Dkt. Mustafa ameeleza kuwa baada ya ukarabati, hospitali hiyo kwa sasa ina vyumba vya VIP vya gharama ya shilingi 40,000 kwa siku, shilingi 20,000 kwa siku na kuna wodi za kawaida ambazo pia zimekarabatiwa kwa shilingi 12,000 kwa siku.

Wakati huo huo, Dkt. Rashid Mfaume alifanya ziara pia kukagua ujenzi katika Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Bunda ambapo baada ya ukaguzi ameitaka Halmashauri kuendelea kukamilisha majengo yaliyobakia ili kuweza kutoa huduma kwa wananchi.  

Katika ziara hiyo, Dkt, Mfaume aliambatana na Wakurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Musoma na Wilaya ya Bunda; maafisa kutoka TAMISEMI, maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na Halmashauri za Manispaa ya Musoma na Wilaya ya Bunda.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa