• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TAKUKURU yafanikisha kijiji cha Seka kulipwa deni

Posted on: November 15th, 2024

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mara kupitia programu yake ya TAKUKURU Rafiki imesaidia Kijiji cha Seka kilichopo katika Kata ya Nyamrandirira, Halmashauri ya Wilaya ya Musoma kulipwa kwa deni la shilingi 37,500,000 kutoka katika mgodi wa MMG Gold Limited kwa ajili ya uwajibikaji wa jamii.

Akitoa taarifa ya robo ya kwanza kwa waandishi wa Habari, Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mara Bwana Mohamed Shariff leo tarehe 15 Novemba, 2024 amesema makubaliano kati ya mgodi huo na Kijiji cha Seka yalikuwa kila mwezi Kijiji kilipwe shilingi 1,500,000 kwa ajili ya kugharimia shughuli za utawala.

“Wakati kero hii inaibuliwa mgodi ulikuwa unadaiwa shilingi 40,500,000 ambazo zilikuwa hazijalipwa kwa muda wa zaidi ya miaka mitano, baada ya TAKUKURU Mkoa wa Mara kufanya ufuatiliaji mwekezaji amelipa shilingi 37,500,000 katika deni hilo” amesema Bwana Shariff.

Bwana Shariff amesema awali Mgodi wa MMG ulidai haukuwa na fedha za kulipa lakini baadaye ukalipa fedha hizo kwenye akaunti ya Kijiji cha Seka na Kata ya Nyamrandirira ambao ndio wanufaika wa fedha za uwajibikaji kwa jamii kwa mujibu wa mkataba uliopo baina ya Kijiji cha Seka na Mgodi wa MMG.

Katika hatua nyingine TAKUKURU imefanya ufuatiliaji wa miradi inayotekelezwa na Serikali na kufanikiwa kudhibiti wizi wa mabati 104 yenye thamani ya shilingi 4,576,000 katika mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari Chifu Sarota baada ya mzabuni kuwasilisha mabati 696 badaya ya mabati 800 yaliyonunuliwa.

Bwana Shariff ameeleza kuwa TAKUKURU imefuatilia miradi ya maendeleo 32 yenye thamani ya shilingi 43,550,103,153.23 katika sekta za afya, elimu, barabara na maji na kati ya hiyo miradi minne yenye thamani ya shilingi 655,159,402 ilikutwa na dosari na hatua zimechukuliwa miradi hiyo imerekebishwa.

Bwana Shariff amesema TAKUKURU ilifanya ufuatiliaji wa mabaraza ya ardhi ya kata katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime na kubaini mabaraza hayo yakitoa hukumu katika mashauri ya ardhi badala ya kutekeleza mabadiliko ya sheria namba 3 ya mwaka 2021 inayotoa mamlaka ya kusuluhisha tu na sio vinginevyo.

“TAKUKURU iliwasiliana na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime ambaye alitoa katazo kwa kuwaandikia barua Watendaji wa Kata kusitisha mabaraza hayo kutoa hukumu” amesema Bwana Shariff.

Bwana Shariff ameeleza kuwa TAKUKURU imefanikiwa kutoa elimu kupitia klabu za wapinga rushwa 56 kutoka shule za msingi, Sekondari na vyuo vya kati na mikutano ya hadhara 61, maonesho 9, vipindi vya redio vinne na semina 31.

Wakati huo huo, TAKUKURU Mkoa wa Mara imeendelea kudhibiti vitendo vya rushwa kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa kuwaelimisha wadau wa uchaguzi na wananchi kutojihusisha na vitendo vya rushwa wakati wa uchaguzi.

Bwana Shariff amesema katika kipindi hicho wamepokea malalamiko 93 na kati ya hayo malalamiko 56 yalihusu rushwa, 37 hayahusu rushwa na kuongeza kuwa malalamiko ambayo yalikuwa hayahusu rushwa watoa taarifa walishauriwa sehemu sahihi ya kuyapeleka.

 Aidha, TAKUKURU imeendesha jumla ya kesi 21 mahakamani ambapo kesi mpya ni tisa na kesi za zamani ni 12 na kesi saba zimeamuliwa ambapo Jamhuri imepata ushindi wa kesi sita na kesi moja imeondolewa mahakamani.  

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa