• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TAKUKURU kuchunguza fedha za Uwajibikaji kwa Jamii Serengeti

Posted on: August 11th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mara kuchunguza matumizi ya fedha za uwajibikaji kwa jamii (CSR) zinazotolewa na Jumuiya ya Uhifadhi wa Wanyamapori (WMA) katika vijiji vitano vya pori la akiba la Ikoma pembezoni mwa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Mheshimiwa Hapi ametoa maagizo hayo leo tarehe 10 Agosti 2021 katika nyakati tofauti baada ya kubaini kuwa ndani ya miaka mitano vijiji hivyo vimepewa shilingi bilioni 4.1 na pesa hizo kutumika katika miradi ambayo haijatekelezwa vizuri.

“Ninataka uchunguzi wa kina wa vijiji hivi ili tuweze kubaini matumizi ya fedha hizi za CSR na wahusika waweze kuchukuliwa hatua za kisheria kutokana na ufisadi pamoja na uzembe uliofanyika hapa” alisema Mheshimiwa Hapi.

Katika miradi hiyo Mheshimiwa Hapi amekuta matumizi ya fedha ni makubwa ikilinganishwa na kazi iliyofanyika, baadhi ya miradi haijakamilika na fedha zimeisha, baadhi ya miradi kutengenezwa chini ya viwango na kadhalika.  

Mheshimiwa Hapi amewataka Wakuu wa Vitengo na Idara pamoja na watumishi wa  Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti kutimiza wajibu wao kwa weredi na ufanisi ili kuendelea kubakia katika utumishi na nyadhifa hizo.  

Aidha amemtaka Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Dkt. Vincent Mashinji na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti Bwana Kivuma Khamis Msangi kusimamia utendaji wa watumishi na kuvunja makundi yote yaliyokuwepo awali.

Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa WMA Bwana Yusuph Manyanda ameeleza kuwa jumuiya yake imekuwa ikitoa fedha kulingana na makusanyo yake ya mwaka kwa serikali za vijiji vinavyoizunguka jumuiya hiyo.

“Mwaka 2017/2018 tulitoa milioni 298; 2018/2019 tulitoa shilingi milioni 262; 2019/2020 tulitoa milioni 193 na mwaka 2020/2021 tulitoa shilingi milioni 81 kwa kila kijiji” alisema Bwana Manyanda.

Bwana Manyanda ameeleza kuwa juma ya fedha iliyopelekwa kwenye vijiji hivyo kama fedha za uwajibikaji kwa jamii ni shilingi bilioni 4.1 ambapo vijiji vilitumia fedha hizo kutekeleza miradi mbalimbali waliyoamua kuitekeleza chini ya usimamizi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wialaya ya Serengeti.

Aidha Bwana Mayanda ameeleza kuwa fedha hizo zilikuwa zikitolewa kila mwaka na kuanzia mwaka jana imepungua kutokana na athari za ugonjwa wa UVIKO 19 katika sekta ya utalii hapa nchini.

Amevitaja vijiji vinavyohusika katika tukio hilo ni vijiji vya Park Nigoti, Robanda, Makundusi, Nichoka na kijiji cha Ikoma.

Mheshimiwa Hapi leo ameendelea na ziara yake katika siku ya pili ambapo ametembelea miradi wa ujenzi wa madarasa, maji na bwalo la chakula na kuzungumza na wananchi katika Shule ya Sekondari ya Robanda; mradi wa maji katika Kijiji cha Makundusi; kufanya mkutano na wananchi katika eneo la omahe,

Aidha Mheshimiwa Hapi ametembelea Shule ya Sekondari ya Makundusi na kuzungumza na viongozi mbalimbali na watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti katika Shule ya Sekondari ya Nuru iliyopo katika mji wa Mugumu.

Kesho Mheshimiwa RC ataendelea na ziara yake katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime ambapo atakagua kwa siku mbili.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa