• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Simbachawene azindua iradi Rorya

Posted on: October 8th, 2024

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Boniface Simbachawene leo tarehe 2 Oktoba, 2024 amefanya ziara katika Wilaya ya Rorya na kutembelea, kukagua kuzindua na kuweka jiwe la msingi katika miradi ya maendeleo.

Miradi iliyotembelewa katika ziara hiyo ni mradi wa ujenzi wa ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Rorya ambao utakapokamilika utakuwa na thamani ya shilingi bilioni 1.25 ambao umewekewa jile la msingi na mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Ingri yenye thamani ya shilingi milioni 540 ambayo imezinduliwa. 

Kabla ya kutembelea miradi hiyo, Mhe. Simbachawene ametembelea Ofisi za Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Rorya na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Rorya ambapo alifanya kikao cha ndani na kusomewa taarifa ya Wilaya.

Akizungumza katika mradi wa shule ya Sekondari ya Ingri, Mkuu wa Wilaya ya Rorya Mhe. Dkt. Khalfany Haule amesema kabla ya ujenzi wa shule hiyo, wanafunzi walikuwa wanatembea zaidi ya kilomita 12 kwenda shule na kurudi katika shule ya Serikali iliyokuwepo eneo hilo.

Mhe. Haule amesema shule hiyo yenye thamani ya shilingi milioni 540 ujenzi wake umekamilika na tayari imesajiriwa na kuanza kuchukua wanafunzi wa kidato cha kwanza kuanzia Januari, 2024 na kwa sasa ina wanafunzi 120.

Akitoa taarifa ya shule hiyo, fedha za ujenzi wa shule hiyo zilipokelewa mwaka 2022/2023 jumla ya shilingi 584,228,028.00 na mradi huo ulitekelezwa kwa njia ya force account na kusimamiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Rorya.

Taarifa hiyo imeonyesha kuwa majengo yaliyojengwa mpaka sasa ni vyumba vya madarasa 8, ofizi za walimu 2, vyumba vitatu vya maabara, chumba cha Tehama, jengo la utawala, maktaba na matundu 12 ya vyoo vya wanafunzi.

Taarifa imeonyesha kuwa kukamilika kwa mradi huu kumesaidia kupunguza msongamano wa wanafunzi katika Shule ya Sekondari ya Mirare ambapo awali wanafunzi wa eneo hilo waliokuwa wanasoma.  

Akitoa taarifa ya mradi wa ukumbi, Kaimu Mkuu wa Idara ya Uhandisi, Mhandisi Ramadhani Mcharo  amesema Halmashauri imepokea shilingi milioni 750 ambazo imetumia kutekeleza mradi huo na kwa sasa ujenzi wa ukumbi huo umefikia asilimia 93.

Mhandisi Mcharo amesema ujenzi wa mradi huo umesaidia kuwezesha vikao vya madiwani kufanyika katika ukumbi huo pamoja na shughuli nyingine za Serikali.

Mhandisi Mcharo amesema kwa sasa Halmashauri inasubiria fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa shughuli zilizobakia ikiwa ni pamoja na ufitishaji wa top za milango, handrails katika ngazi, kumwaga jamvi, mfumo wa umeme awamu ya pili, Tehama, sauti, mfumo wa maji awamu ya pili, na uwekaji wa samani katika jengo hilo.

Baada ya ukaguzi wa miradi Mhe. Simbachawene alifanya mkutano wa hadhara katika eneo la utegi na baada ya hapo alielekea Tarime kuendelea na ziara yake.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa