• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Shule bora yatoa mafunzo ufundishaji kiingereza

Posted on: December 19th, 2023

Walimu Wakuu na Maafisa Elimu Kata ambao shule zao zilifanya vibaya kwenye Somo la Kiingereza katika mtihani wa Taifa wa Darasa la Saba mwaka 2023 Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti leo tarehe 27 Novemba, 2023 wamepewa mafunzo ya namna ya kusimamia ufundishaji wa somo hilo yaliyofanyika katika Shule ya Msingi Azimio A. 

Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo hayo, Mwakilishi wa Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu Bwana Mujibu Mustafa Babara ameeleza kuwa mafunzo hayo ni muhimu na kuwataka washiriki wa mafunzo kufuatilia mafunzo hayo ili kwenda kubadilisha hali ya ufundishaji wa somo hilo.

“Tunataka mkimaliza mafunzo hayo, mabadiliko ya wazi yaonekani kwa namna walimu wenu watakavyokuwa wanafundisha na namna wanafunzi watakavyoongeza ufaulu wa asomo la kiingereza katika shule zenu” amesema Bwana Babara.

Bwana Babara ameeleza kuwa kwa Mkoa wa Mara wataalamu hao watakuwa wakwanza kupewa mafunzo ya kusimamia na kutekeleza muhutasari wa somo la Kiingereza kwa shule za Msingi kulingana na Mtaala wa Elimu ya Msingi, 2023.

“Ninyi mnapewa mafunzo kwenye mada mpya kabisa ambayo nina uhakika sio walimu wote hapa nchini watapata fursa mliyoipata leo, tuyatendee haki haya mafunzo na tukawajibike katika kuwasimamia walimu wanaofundisha” amesema Bwana Babara.

Kwa upande wake Mratibu wa Mradi wa Shule Bora Bwana Sam Mwita ameeleza kuwa ufaulu wa somo la Kiingereza kitaifa ni asilimia 34 na Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti ilikuwa ni ya mwisho katika matokeo ya mtihani wa Taifa wa Darasa la Saba, 2023.

“Ni mategemeo yetu kuwa mafunzo haya, na mafunzo yatakayotolewa kwa waliu kesho yataboresha ufundishaji wa wanafunzi na hivyo kuja kuboresha matokeo ya somo la kiingereza katika mitihani ya ndani na mitihani ya Taifa” amesema Bwana Mwita.

Bwana Mwita ameelezea imani yake kuwa walimu hao wanaouwezo wa kufanya mabadiliko na wanasifa za kufanya mabadiliko na kuwataka kutekeleza kwa ufanisi mpangokazi watakaotoka nao katika mafunzo hayo.

Kwa upande wake, Mdhibiti Ubora wa Kanda ya Ziwa Bibi Lucy Nyanda ameeleza kuwa kuna mabadiliko makubwa katika Sekta ya Elimu na hivyo walimu hawana budi kujifunza kuhusu mtaala na sera mpya za elimu zilizoanza kutumika hivi karibuni.

Bibi Nyanda amewataka washiriki hao kuchukulia mafunzo hayo kama chachu ya kujifunza mambo yote yanayohusiana na elimu na mabadiliko ya mitaala na sera ili kuweza kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Mafunzo ya Wakuu wa Shule na Maafisa Elimu Kata yanatarajiwa kufuatiwa na mafunzo kwa walimu wanaofundisha somo la Kiingereza katika shule hizo yanayotarajiwa kufanyika kwa siku tatu kuanzia tarehe 28 Novemba, 2023.

 Mafunzo haya yanatolewa na Wakala wa Maendeleo ya Elimu (ADEM) na kufadhiliwa na Mradi wa Shule Bora.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa