• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Serikali yatoa maamuzi matumizi ya CSR Tarime

Posted on: July 13th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi leo tarehe 13 Julai, 2022 ametoa mrejesho wa maamuzi ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb.) kuhusu fedha za uwajibikaji kwa jamii (CSR) zinazotolewa na Mgodi wa Dhahabu wa Barrick North Mara.

Akizungumza katika kikao cha Baraza Maalum la Madiwani la kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa maamuzi ya Waziri Mkuu yalitolewa katika kikao cha pamoja kilichowahusisha viongozi wa serikali wa ngazi mbalimbali, Mbunge wa Tarime Vijijini na viongozi wa Mgodi wa Barrick North Mara.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa maamuzi ya kikao hicho yalikuwa fedha zote za CSR zinazotolewa na mgodi huo ni mali ya umma na matumizi ya fedha hizo lazima yafuate taratibu zote za fedha za Serikali za mitaa. 

“Serikali imeamua kuwa hakutakuwa tena na Kamati ya Maendeleo ya Jamii (CDC) iliyokuwa ikitumika  kupanga na kutekeleza miradi ya CSR katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime na badala yake miradi yote itatekelezwa kwa mujibu wa taratibu na miongozo ya kawaida ya serikali” alisema Mheshimiwa Hapi.

“Wataalamu watapata fursa ya kuchambua miradi iliyoibuliwa na kufanya michakato ya kitaalamu kuhusiana na miradi hiyo kabla ya kuiwasilisha kwenye mamlaka za maamuzi kwa ajili ya kuidhinisha utekelezaji wa miradi hiyo” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mfumo wa malipo ya fedha hizo itakuwa sawa na fedha zote za Serikali na zitapelekwa kwenye Kata ambapo mradi unatekelezwa na taratibu zote za fedha na manunuzi ya umma zitafuatwa katika utekelezaji wa miradi hiyo.

Mkuu wa Mkoa ameeleza kuwa kuanzia sasa Serikali kwa maana ya Mkoa na Halmashauri utashiriki kwenye kukokotoa kiwango cha CSR kitakacholipwa na mgodi kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Tarime sio kama ilivyokuwa awali halmashauri ilikuwa ikipatiwa taarifa tu na mgodi kuhusu kiasi cha CSR.  

Aidha, Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa fedha ya CSR itatolewa kwa Dola za Kimarekani na Halmashauri ndio itakayehusika katika kubadilisha dola hizo kuwa fedha za kitanzania kwa ajili ya matumizi ya Halmashauri.

“Huu utaratibu wa matumizi ya CSR umekubalika kuwa ni utaratibu wa nchi nzima baada ya kikao kilichofanyika chini ya usimamizi wa Waziri Mkuu” alisema Mheshimiwa Hapi.

Maamuzi haya ya Serikali yanahitimisha malumbano ya matumizi ya fedha CSR katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime yaliyodumu kwa muda mrefu kufuatia uongozi wa Mkoa wa Mara kuingilia kati matumizi ya fedha hizo na kuunda kamati maalum ambayo iliwasilisha taarifa yake tarehe 20 Aprili, 2022.

Hata hivyo kulikuwepo na malalamiko ya wananchi na wanasiasa hususan baada ya kuvunjwa kwa CDC tarehe 20 Aprili, 2022 na vyombo vya dola kuanza uchunguzi kutokana na tuhuma za ubadhilifu wa fedha za CSR za Halmashauri ya Wilaya ya Tarime.  

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa