• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Serikali kuendelea kuunga mkono shughuli za wanawake hapa nchini

Posted on: February 14th, 2025

Mkuu wa mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo amefungua Mkutano wa Chemba ya Wanawake Wafanyabiashara Mkoa wa Mara na kuwahakikishia kuwa Serikali ya Awamu ya Sita itaendelea kuunga mkono shughuli za wanawake hapa nchini.

Mhe. Mtambi ameeleza hayo leo Februari 14, 2025 katika Ukumbi wa Uwekezaji uliopo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara wakati akizungumza na wanawake takriban 200 wanachama wa Chemba ya Wanawake Tanzania.

“Serikali inazo fursa nyingi kwa ajili ya wanawake ikiwemo mikopo ya asilimia kumi inayotolewa na Mamlaka ya Serikali za Mitaa hapa nchini kwa ajili ya makundi maalum ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu” amesema Mhe Mtambi.

Mhe. Mtambi pia amesema Serikali imeweka mazingira mazuri ikiwemo sera, sheria, kanuni na taratibu zinazowawezesha wanawake kufanya shughuli zao na hususan shughuli za uzalishaji mali bila kubaguliwa.  

Mhe. Mtambi ametumia fursa hiyo pia kuwakumbusha wanawake wa Mkoa wa Mara kuhusu fursa mbalimbali zilizopo katika Mkoa wa Mara ikiwa ni pamoja na kilimo, ufugaji, uvuvi, utalii na uchimbaji wa madini.

Wakati huo huo, Mhe. Mtambi amemuagiza Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara kuhakikisha kuwa katika maonesho ya Kitaifa na Kimataifa wanawake wa Mkoa wa Mara wanapata nafasi na wanashiriki.  

Aidha, Mhe. Mtambi amewataka wanawake wa Mkoa wa Mara kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni pamoja na kuwania nafasi mbalimbali zinazogombaniwa na kupiga kura ili kumchagua Rais, wabunge na madiwani.  

Awali, akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa, Katibu wa Chemba ya wanawake Mkoa wa Mara Bi Anastazia Kirati amesema wanawake wajasiriamali wanapata changamoto katika kupata mikopo kutoka Serikalini na taasisi za kifedha.

“Wanawake wanapata changamoto ya kupata mikopo ambapo wapo wanaopata lakini hawana fursa ya elimu ya kutosha na hivyo kuwafanya kushindwa kuitumia vizuri mikopo hiyo.” Amesema Bi. Anastazia.

Bi. Anastazia ameiomba Serikali na taasisi za kifedha kutoa elimu ya biashara kwa wajasiriamali wanaopewa mikopo ili waweze kufaidika zaidi na mikopo hiyo kwa kuendeleza biashara zao.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kanda wa TWCC Bi Happines Mabula amesema kuwa chemba yao ilianzishwa mwaka 2005 sasa inakaribia kuwa na miaka 20 ikitoa huduma zake kwa wananwake wafanyabiashara na wajasiriamali hapa nchini.

Ufunguzi wa mkutano huo umehudhuriwa pia na baadhi ya maafisa kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mara na Halmashauri ya Manispaa ya Musoma.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa