• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Serikali kuboresha usimamizi wa Mashauri ya Ardhi

Posted on: December 11th, 2024

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini leo amezindua Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia katika Mkoa wa Mara amesema Serikali imeanza mchakato wa kuboresha usimamizi na usikilizaji wa mashauri yanayohusiana na ardhi.

“Mhe. Rais ameziagiza Wizara za Katiba na Sheria, Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Mahakama kukutana ili kuhuisha mfumo wa usimamiaji wa mashauri ya ardhi hapa nchini” amesema Mhe. Sagini.

Mhe. Sagini amesema kwa sasa mfumo wa utoaji haki wa mahakama hapa nchini umeimarika sana na mashauri hayachukui muda mrefu sana kusikilizwa kama katika mabaraza ya ardhi kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ukosefu wa mabaraza katika baadhi ya maeneo ya utawala jambo ambalo linasababisha kero kwa wananchi.  

Akizungumza na wananchi wa Mkoa wa Mara Mhe. Sagini amesema Serikali inaendelea na mchakato ili kuhakikisha mashauri hayo yanafanyika katika mfumo wa kawaida wa Mahakama ili kuboresha utoaji wa huduma za kisheria na utatuzi wa migogoro kwa wananchi.

Mhe. Sagini ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Butiama akizungumzia Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia amesema kampeni hiyo inalenga kuwapatia wananchi elimu juu ya upatikanaji wa huduma za kisheria bila malipo na kutoa mafunzo ya uraia na utawala bora kwa viongozi na watendaji katika nafasi mbalimbali.

Naibu Waziri huyo amesema tangu imeanza kufanyika hapa nchini, wananchi wengi wamejitokeza kuwasilisha malalamiko yao na kuwataka wananchi wa Mkoa wa Marakujitokeza kwa wingi na kutumia fursa hiyo vizuri na hususan inapopita katika maeneo yao.

Mhe. Sagini amesema katika ushughulikiaji wa kesi za mirathi hamna ubaguzi wa wanawake na wanaume katika sheria na dhamira ya Serikali ni kujenga jamii yenye haki sawa kwa watu wote mbele ya sheria na vyombo vya kutoa maamuzi.

Akisoma salamu za Mkoa wa Mara, Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Mara Dkt. Khalfan Haule ameiomba Serikali kufanya maboresho ya namna ya kushughulikia migogoro ya ardhi na hususan uundwaji wa Mabaraza ya Ardhi ya Wilaya.

Mhe. Haule ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Rorya amesema baadhi ya Wilaya za Mkoa wa Mara hazina mabaraza jambo ambalo linalazimisha kutembea umbali mrefu kufuata huduma za mahakama hizo katika Wilaya nyingine.

Mhe. Haule ametoa mfano wa Wilaya za Butiama na Rorya ambazo hazina Mabaraza ya Ardhi na wananchi wake kulazimika kufuata huduma katika wilaya nyingine jambo ambalo linaleta usumbufu kwa wananchi.

Dkt. Haule amesema Mkoa una migogoro mingi ya ardhi na mabaraza ya ardhi yanachelewesha sana utatuzi wa migogoro jambo ambalo linaongeza kero kwa wananchi na kuiomba Serikali kufikiria namna ya kuzitumia mahakama za kawaida kushughulikia migogoro ya ardhi.  

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bwana Daudi James Mirumbe ameupongeza ushirikiano walioupata katika Mkoa wa Mara katika maandalizi ya uzinduzi wa Kampeni hiyo.

Bwana Mirumbe amewapongeza wadau wote waliosaidia kwa hali na mali kufanikisha uzinduzi wa kampeni hiyo katika Mkoa wa Mara kwa mafanikio makubwa na kuwaomba wananchi kutumia fursa hii ya siku tisa kutembelea mabanda ya maonyesho yatakayoendelea kuwepo katika viwanja hivyo.

 Uzinduzi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia umefanyika katika Uwanjwa wa Mukendo, Manispaa ya Musoma ikiwa na kauli mbiu ya kampeni hiyo ni: Msaada wa Kisheria kwa Haki, Usawa, Amani na Maendeleo.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa