• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC Mtambi amtaka mkandarasi kukamilisha mradi wa maji Serengeti kwa wakati

Posted on: July 21st, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 21 Julai, 2025 amefanya ziara katika Wilaya ya Serengeti na kukagua Mradi wa Maji wa Miji 28 katika Mji wa Mugumu na kumtaka mkandarasi Mega Engineering and Infrastructure Company Limited kukamilisha mradi huo kwa wakati.

Akizungumza baada ya kukagua mradi huo, Mhe. Mtambi amesema Serikali imeweka mazingira wezeshi kwa mkandarasi ikiwemo kutoa fedha za kutekeleza mradi huo kwa wakati, hivyo hakuna sababu ya msingi kwa mkandarasi kuchelewesha utekelezaji wa mradi huo.

“Mradi huu ulipaswa kukamilika mwezi Aprili, 2025 na ukaomba kuongezewa muda hadi Desemba, 2025 ninaomba ujue kuwa hakutakuwa na muda wa nyongeza baada ya hapo, mradi huu ukamilike kwa wakati” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema kwa sasa mkandarasi hana madai ambayo hayajalipwa na vifaa vyote vipo katika eneo la mradi na kuwataka wasimamizi wa mradi huo pamoja na mkandarasi kushirikiana na kukamilisha mradi kwa wakati ili wananchi waweze kupata maji safi na salama.

Aidha, Kanali Mtambi ameonyesha kufurahishwa na maendeleo ya mradi huo na kumpongeza mkandarasi kwa kazi zinazoendelea baada ya kuongezewa muda wa utekelezaji wa mradi huo na kumtahadharisha kuwa Serikali haitatoa muda mwingine wa nyongeza katika mradi huo.

Akizungumza kuhusiana na mradi huo, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Musoma (MUWASA) Mhandisi Nicas Mugisha amesema mradi huo unaogharimu shilingi bilioni 21 ulianza kutekelezwa mwezi Aprili, 2023 na unatarajiwa kukamilika Desemba, 2025.

Mhandisi Mugisha amesema kukamilika kwa mradi huo kutasaidia kuondoa adha ya maji kwa watu zaidi ya laki moja wa Mji wa Mugumu katika Wilaya ya Serengeti.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa ameiongoza Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mara kukagua miradi itakayotembelewa na Mwenge wa Uhuru mwaka 2025 katika Wilaya ya Serengeti.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa ameambatana na Kamati ya Usalama ya Mkoa, Kamati ya wataalamu ya Mkoa, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Serengeti na wataalamu mbalimbali kutoka MUWASA na Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa