• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC Mara awataka wananchi kuchukua tahadhari ya MURBUG

Posted on: January 22nd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ameongoza kikao utambulisho wa kazi na majukumu ya Mamlaka ya Kudhibiti Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA) na kuwataka wananchi wa Mkoa wa Mara kuchukua tahadhari na kujilinda dhidi ya tishio la kusambaa kwa maabukizi ya ugonjwa wa murbug hapa nchini.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Mtambi amesema japokuwa kwa sasa tishio la ugonjwa huo sio kubwa lakini wananchi wachukue tahadhari kwa kuwa ugonjwa huo hauna kinga wala tiba na unasababisha vifo kwa asilimia zaidi ya 80 ya wagonjwa wanaopata maambuki ya ugonjwa huo.

“Japokuwa kwa sasa ni mtu mmoja amegundulika katika Mkoa wa Kagera, lakini bado kuna uwezekano wa uwepo wa wagonjwa wengine ambao bado hawajagundulika au huyo mgonjwa anaweza kuwa ameshawaambukiza watu wengine kabla yeye hajagundulika” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amewataka wananchi kuwasikiliza na kufuata maelekezo ya wataalamu wa afya kuhusiana na namna ya kukabiliana na tishio la ugonjwa huo na hususan kuacha baadhi ya tabia za mazoea zilizozoeleka katika jamii na kuanza tena utaratibu wa kunawa mikono maji tiririka na sabuni kila wakati.

Mhe. Mtambi amewataka wataalamu wa afya, Wakuu wa Wilaya na viongozi wa Halmashauri kuendelea kutoa elimu kwa wananchi pamoja na kutoa miongozo ya namna ya kukabiliana na tishio la kuenea kwa ugonjwa huo hapa nchini.  

Kwa upande wake, mwakilishi wa Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Afya, Lishe, Ustawi wa Jamii Bwana Erick Yossam Muhigi amesema amesema Mkoa wa Mara unaendelea na utoaji wa Elimu kwa wananchi kuhusiana na ugonjwa wa Murbug na hususan baada ya kugundulika mgonjwa mmoja katika Mkoa wa Kagera.

Bwana Muhigi amezitaja dalili za ugonjwa wa murbug kuwa ni pamoja na muathirika kupata homa kali, kuharisha, kuharisha damu, kutapika, kutapika damu na kutokwa na damu katika sehemu mbalimbali mwilini.

“Ugonjwa huu unaenea kwa njia mbalimbali ikiwemo kugusa jasho, mkojo, damu, kinyesi, matapishi, nguo, matandiko, kugusana na mtu aliyeathrika na ugonjwa huo au wanyama walioathirika na ugonjwa huo” amesema Bwana Muhigi.

Bwana Muhigi amewataka wananchi kuchukua tahadhari kwa kunawa maji tiririka na sabuni, kuepuka kugusa au kuosha maiti ya mtu aliyoathirika na ugonjwa huo na kuepuka kula mizoga ya wanyama waliokufa kutokana na uwezekano wa kula nyama ya mnyama aliyeathrika na ugonjwa huo.

Bwana Muhigi amesema ugonjwa huu unasambaa kwa haraka katika jamii na mtu ambaye ameathirika na ugonjwa huu anaanza kuonyesha dalili za kuwa na ugonjwa wa murbug baada ya siku mbili hadi 21 na muathirika huyo anaweza kuwaambukiza wengine hata kama hana dalili za ugonjwa huo jambo ambalo linaongeza kusambaa kwa maambukizi katika jamii.

Bwana Muhigi amesema Mkoa wa Mara umeimarisha udhibiti wa wagonjwa katika mpaka wa Sirari na vivuko vya wananchi kupita kutoka nchi jirani, udhibiti wa Uwanja wa Ndege wa Musoma na viwanja vigine vya ndege vilivyoko katika Mkoa wa Mara.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Wakuu wa Wilaya, Kamati ya Usalama Mkoa, viongozi wa dini, viongozi wa vyama vya siasa, maafisa kutoka taasisi mbalimbali, Halmashauri za Mkoa wa Mara, wadau wa kilimo, mifugo na biashara Mkoa wa Mara.  

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa