• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC azindua mradi wa Utafiti unaofadhiliwa na IRDC

Posted on: November 15th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee leo amezindua mradi wa utafiti wa “Kuhamasisha Uanzishaji wa Ajira na Miradi ya Kiuchumi kwa Vijana, Wanawake na Watu wenye Ulemavu” unaofadhiliwa na Kituo cha Kimataifa cha Utafiti wa Maendeleo (IRDC) cha Canada.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mheshimiwa Mzee amewataka watafiti hao kuhakikisha wanaufanya utafiti huo na kutoa matokeo ya utafiti huo kwa haraka ili Serikali ikiyafanyia kazi mapungufu yaliyopo iweze kuwasaidia wananchi.

“Matokeo ya utafiti huu tunatarajia yapunguze athari za mapungufu yanayoendelea kwa sasa katika utoaji wa mikopo ya makundi maalum kwa Halmashauri zetu, sasa yakichelewa sana hayatakuwa na manufaa tunayoyatarajia” alisema Mheshimiwa Mzee.

Aidha, ametoa changamoto kwa Chuo Kikuu cha Mwalimu Julius K. Nyerere cha Kilimo na Teknolojia kuhakikisha wasomi watakaopita katika Chuo hicho wanajiajiri na wanaajiri wengine ili kupunguza uhaba wa ajira hapa nchini.

Kwa upande wake Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo cha Mwalimu Julius K. Nyerere cha Kilimo na Teknolojia (MJNUAT) Prof. Lesakit Mellau ameeleza kuwa mradi huo utafanyika katika kipindi cha miaka mitatu na gharama ya mradi mzima ni shilingi milioni 910.

Prof.Mellau ameeleza kuwa mradi huo unaunganisha mafunzo kwa wahadhiri watatu mmoja katika Shahada ya Uzamivu na wawili katika Shahada ya Uzamili pamoja na utafiti utakaofanyika katika Mikoa ya Mara na Arusha.

Ameeleza kuwa kwa Mkoa wa Mara utafiti utafanyika katika Halmashauri  ya Wilaya ya Butiama, Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti, Halmashauri ya Mji wa Bunda, Manispaa ya Musoma, Halmashauri ya Wilaya ya Bunda,  na Halmashauri tatu za Mkoa wa Arusha ambazo ni Halmashauri ya Jiji la Arusha, Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro na Halmashauri ya Wilaya ya Longido.

Prof. Mellau ameeleza kuwa dhima ya Chuo hicho ni Pata Elimu, Jiajiri, Tengeneza Ajira ambayo inalengo la kuhamasisha wanachuo wa Chuo hicho kusoma kwa bidi ili kuja kujiajiri na kutengeneza ajira za kuajiri watu wengine.

Uzinduzi wa utafiti huo umehudhuriwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha, wataalamu wa Chuo hicho, Wakurugenzi wa Halmashauri zitakazopitiwa na utafiti, mashirika yasiyo ya kiserikali na watafiti watakaohusika katika Mradi huo.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa