• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC awataka wananchi wa Nyanungu kutumia fursa vizuri

Posted on: February 10th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee leo amewataka waanchi wa Kata ya Nyanungu, katika Wilaya ya Tarime kulitumia vizuri eneo la mlima linalopakana na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti (SENAPA) kwa maendeleo ya uhifadhi na utalii na kuacha mara moja shughuli za kilimo.

Mheshimiwa Mzee amesema hayo kwa nyakati tofauti tofauti wakati alipoambatana na viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Kamati ya Usalama ya Mkoa na Wilaya ya Tarime kukagua eneo hilo kwa lengo la kusuluhisha mgogoro baina ya wananchi na SENAPA.  

“Mkilitumia eneo hili kwa kuwaita wawekezaji wa kujenga hoteli za kitalii, mtakuwa matajiri na mtaachana na migogoro baina yenu na watumishi wa SENAPA waliokasimiwa na Taifa kuilinda Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ” amesema Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee amewataka wananchi hao kuangalia mfano wa nchi ya Kenya ambayo imetumia eneo lilalopakana na mlima huo kwa upande wa Tanzania kuweka vivutio vya watalii na kulitumia vizuri eneo lao.  

“Tuangalie majirani zetu tunaopakana nao hapa, wao wanalitumia eneo lao kwa ajili ya shughuli ya utalii, na katika eneo lao Serengeti haionekani vizuri kama ukiwa hapa tulipo, lakini sisi hapa tunalima humu kwenye mawe na tunachokipata hakina tija hata kwa mkulima mwenyewe” amesema Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee amewataka wananchi kuheshimu mpaka kati ya vijiji hivyo na SENAPA ili kuepusha migogoro ya mara kwa mara katika eneo hilo na badala yake wajikite kwenye kujenga mahusiano na ujirani mwema na SENAPA.

Wakati huo huo, Mheshimiwa Mzee amekemea kitendo cha wananchi wa eneo hilo kumuua askari wa SENAPA kwa mshale wa sumu akiwa katika eneo la Hifadhi akitekeleza majukumu yake na kuwakemea wanasiasa wanaowahamasisha wananchi kutembea umbali mrefu ndani ya hifadhi ili kunywesha mifugo katika Mto Mara uliopo ndani ya hifadhi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mara Mheshimiwa Patrick Chandi Marwa amewasihi wananchi kuitumia fursa hiyo vizuri na kuliomba Shirika la Hifadhi za Tanzania (TANAPA) kuwapeleka wawekezaji wakubwa katika eneo hilo.

“Mwekezaji huyo aingie mkataba na vijiji hivi ili mapato yanayotokana na uwekezaji huo yabadilishe maisha ya wananchi wa eneo hili na kuachana na migogoro isiyokuwa na tija” amesema Mheshimiwa Chandi.

Mheshimiwa Chandi amewapa mfano wa Kijiji cha Natta kilichopo katika Wilaya ya Serengeti ambacho  ambacho kina milima miwili midogo kuliko Nyanungu na wananchi wameruhusu uwekezaji na sasa Kijiji kinapata shilingi bilioni tatu kila mwaka kutoka kwa uwekezaji huo.

 

Eneo la vijiji vitano katika Kata ya Nyanungu vipo katika mlima wenye madhari ya kipekee unaowezesha watu kuitazama sehemu kubwa ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na na hivyo kufaa kwa ajili ya uwekezaji wa hoteli za kitalii.  

 Taarifa iliyotolewa na wataalamu wa TANAPA inaonyesha kuwa kufuatia maagizo ya Baraza la Mawaziri kuhusu matumizi ya eneo la kinga (buffer zone) katika vijiji vitano vya Kata ya Nyanungu, vijiji vya Kegonga na Nyandage vimegomea kuwekewa vigingi vya mpaka wakati vijiji vya Gibaso, Masanga na Karakatonga wamekubali kuwekewa alama za mipaka na kuruhusu kupimiwa eneo lao.  

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa