• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC awaomba viongozi wa dini kulinda maadili ya jamii

Posted on: March 28th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Evans Alfred Mtambi leo tarehe 27 Machi, 2025 ameandaa futari kwa ajili ya mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani na kuwataka viongozi wa dini kuisaidia Serikali katika kulinda maadili katika jamii na amani na utulivu kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Akizungumza na washiriki wa futari hiyo iliyofanyika nyumbani kwake katika Mtaa wa Mukendo, Manispaa ya Musoma, Mhe. Mtambi amewataka viongozi wa dini kukemea mmomonyoko wa maadili katika jamii ili kuijenga jamii yenye maadili mema.

“Tuwakumbushe waumini wetu kuhusu kufuatilia maadili ya watoto katika jamii yetu ili kujenga kizazi chenye maadili mema na kuwafanya watu kuwa na hofu ya Mungu katika maisha yao” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amewataka viongozi wa dini kukemea malezi yanayofanywa na mitandao ya kijamii na badala yake amewataka viongozi hao kuwahamasisha waumini wao katika kuwajibika katika malezi kama wazazi na walezi wa watoto na sio kuiachia mitandao ya kijamii.

Mhe. Mtambi amewataka viongozi wa dini kuhamasisha amani na utulivu uliopo katika nchi yetu uendelee hata wakati wa uchaguzi mkuu ili uchaguzi ufanyike kwa amani na utulivu na usiwe kama njia ya kuhalalisha uhalifu kwa watu wanaopenda kufanya hivyo.  

Kanali Mtambi amewataka viongozi wa dini kukemea vitendo vyovyote vya kuvuruga amani wakati wa uchaguzi na baada ya uchaguzi na kuwataka kuombea amani, umoja na ushirikiano kwa wananchi wote ili nchi yetu ijikite zaidi katika kutekeleza shughuli za maendeleo na sio mapigano.

Mhe. Mtambi amewataka viongozi wa dini kuendelea kuwaombea viongozi na amani ya nchi ya Tanzania ili iendelee kuwepo na kuuombea Mkoa uweze kuepukana na majanga mbalimbali na uweze kufanya vizuri katika shughuli za maendeleo.

Mkuu wa Mkoa amewataka viongozi wa dini kuwahamasisha wazazi kuhusu elimu ya watoto wao na kutoa mfano mwaka 2025 wanafunzi wa kidato cha kwanza wengi hawakuanza shule hadi Serikali ya Mkoa ilipowafuatilia wazazi na walezi wa wanafunzi hao.

“Pamoja na uwekezaji wa Serikali katika elimu, bado wazazi wengi hawana mwamko wa kuwapeleka watoto wao shule jambo ambalo linaufanya uwekezaji huu uwe ni kazi bure, sisi kama Serikali hatutakubali” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema kutokumpeleka mtoto shule, kutochangia chakula ili mtoto ale akiwa shuleni ni ukatili kwa watoto kwa sababu unawanyima watoto haki yao ya msingi ya kupata elimu.

Aidha, Mhe. Mtambi amewataka viongozi wa dini kukemea mila za ukeketaji, jamii kujichukulia sheria mkononi, ubabe usio na msingi na kusema kuwa kwa Mkoa wa Mara mambo kama hayo yamepitwa na wakati na badala yake viongozi wa dini wahamasishe waumini kushiriki katika shughuli za maendeleo ili kuuinua Mkoa wa Mara kiuchumi.

Futari hiyo pamoja na viongozi wa dini ilihudhuriwa pia na Kamati ya Usalama ya Mkoa, viongozi wa ngazi mbalimbali, taasisi za umma na taasisi binafsi na wawakilishi wa waumini wa dini na madhehebu mbalimbali.  

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa