• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC awahimiza wafanyakazi ushirikiano

Posted on: August 31st, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee leo amekutana na wafanyakazi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na kuwataka wafanyakazi kuongeza ushirikiano baina ya wafanyakazi na viongozi ili kuweza kutatua changamoto zinazowakabili wananchi wa Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Mzee amesema kuwa kwa kawaida wafanyakazi wanatumia muda mwingi ofisini, kwa hiyo ni muhimu ofisini kuwe ni mahali pazuri kwa ajili ya kuishi, kwenye ushirikiano wa kutosha ili watu wafanye kazi zao kwa furaha.

“Mimi nimekuja kwa ajili yenu, mimi ni mtumishi wenu, mkifanya vizuri katika majukumu yenu mimi nitapewa sifa, lakini mkiharibu na mimi mtaniharibia pia, kwa hiyo tujitahidi kufanya kazi vizuri na kwa ushirikiano ili tuweze kuyafikia malengo yetu” alisema Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee amewashukuru wafanyakazi wa Ofisi a Mkuu wa Mkoa wa Mara kwa mapokezi mazuri waliyompa wakati alipowasili kwa ajili ya kuanza kazi katika Mkoani Mara tarehe 6 Agosti, 2022.

Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa anapenda kuona mabadiliko yenye a kimaendeleo katika utendaji kazi na kuwahudumia wananchi wa Mkoa wa Mara.

Amewapa changamoto wafanyakazi kutafuta mradi au shughuli ya kiuchumi ya kufanya kwa pamoja itakayowaongezea wafanyakazi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na familia zao kipato ili waweze kujikimu kimaisha.

Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa anatamani atakapoondoka Mkoa wa Mara awe ameacha alama, na hiyo hawezi kufanya peke yake anahitaji ushirikiano wa watumishi wote katika kufanikisha azma yake ya kuiletea Mara maendeleo.

Mkuu wa Mkoa ameeleza kuwa katika kufanya kazi atawashirikisha wafanyakazi wote na kuongeza kuwa “kuweni huru na mimi, mtu akifanyakazi yake vizuri hatuwezi kugombana na tukiwa kwenye misingi ya kazi hatuwezi kuwa maadui” alisema Mheshimiwa Mzee.

Kwa upande wake, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Dominicus Lusasi ameeleza kuwa kwa sasa Mkoa wa Mara una wafanyakazi 178 ambao kati yao wafanyakazi 88 wapo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na wengine wapo katika ofisi za Wakuu wa Wilaya na ofisi za Maafisa Tarafa.

Bwana Lusasi ameeleza kuwa kwa sasa ofisi ya Mkuu wa Mkoa ina jumla ya Idara saba na vitengo sita kwa mujibu wa muundo mpya wa utumishi ulioanza kutumika katika Sekretarieti za Mikoa hapa nchini kuanzia tarehe 1 Julai, 2022.

Bwana Lusasi amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kutenga muda wa kuzungumza na watumishi na kuahidi kuyafanyia kazi maelekezo aliyoyatoa.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa