• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC atoa siku 14 wanafunzi wote Sekondari ya J. K. Nyerere wapate chakula shuleni

Posted on: July 28th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 28 Julai, 2025 amefanya ziara Wilaya ya Tarime na kumtaka Mkuu wa Wilaya ya Tarime kuhakikisha wanafunzi wote wa Shule ya Sekondari ya J. K. Nyerere iliyopo Nyamwaga, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime wanapata chakula cha mchana wakiwa shuleni.

Mhe. Mtambi ametoa agizo hilo wakati akizungumza na wanafunzi wa kidato cha pili wa shule hiyo baada ya kupokea taarifa kuwa wanafunzi wanaosoma kutwa wa kidato cha kwanza hadi cha nne ambao wazazi wao wamechangia chakula tu ndio wanaopewa chakula shuleni.  

“Ninatoa siku 14 Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Tarime hakikisha wanafunzi wote wa shule hii ikiwemo na hawa wanaosoma kutwa wanapata chakula cha mchana wakiwa shuleni, hali hii haikubaliki” amesema Mhe. Mtambi.

Aidha, Mhe. Mtambi amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime kutoa chakula cha mchana kwa wanafunzi wote wa kidato cha pili wa shule hiyo wanaoendelea na mtihani wa upimaji wa kidato cha pili Kimkoa ulioanza leo katika Mkoa wa Mara.

“Mkurugenzi wapatie chakula cha mchana hawa wanafunzi wanaofanya mtihani mpaka mtihani wao utakapoisha ili waweze kufanya vizuri katika mtihani wao” ameagiza Mhe. Mtambi.

Akizungumza katika eneo hilo, Mkuu wa Shule ya Sekondari ya J. K. Nyerere Mwalimu Melesiana Julius Gerald amesema kuwa uongozi wa shule pamoja na Halmashauri hiyo umefanya jitihada mbalimbali kuhakikisha wanafunzi wote wanapata chakula shuleni.

Mwalimu Gerald amesema kwa sasa wanafunzi wote wa kidato cha tano na sita ambao wanakaa bwenini wanapata chakula hata hivyo baadhi ya wanafunzi wa kidato cha kwanza hadi cha nne wanaosoma kutwa katika shule hiyo hawapati chakula shuleni.  

“Kwa sasa ni kama robo tatu ya wanafunzi wanaosoma ndio wanapata chakula shuleni na wengine hawapati chakula kutokana na ugumu wa wazazi kuchangia chakula kwa ajili ya watoto wao” amesema Mwalimu Gerald.  

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo amekabidhi mizinga ya kufugia nyuki 121 iliyotolewa na wadau mbalimbali kwa Baraza la Wazee pamoja na wazee wa mila wa koo 12 za Kabila la Wakurya wa Wilaya ya Tarime na kuwahakikishia wazee kuwa Serikali inauthamini sana mchango wao katika jamii.

Akizungumza katika tukio hilo, Mhe. Mtambi amesema lengo la kuwapa mizinga hiyo ni kuanzisha miradi wa ufugaji nyuki katika misitu iliyopo katika Wilaya ya Tarime jambo ambalo litawaweka wazee hao kuwa karibu na misitu ambayo wamekuwa wakiitunza katika maisha yao yote.

Mhe. Mtambi ametumia fursa hiyo kuwahamasisha wazee hao kushiriki uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 kwa kupiga kura na kuihamasisha jamii kupiga kura ili kupata haki yao ya kikatiba ya kuwachagua viongozi watakaowaongoza katika nafasi mbalibmbali ikiwemo Rais, Wabunge na Madiwani.

Kanali Mtambi amewashukuru wadau wote waliochangia kufanikisha wazee hao kupata mizinga ya kufugia nyuki ambayo itawasaidia kuanzisha mradi wa kuwainua kiuchumi na kuwaeleza kuwa Serikali imeendelea kuboresha upatikanaji wa huduma mbalimbali kwa wazee.  

Aidha, Mhe. Mtambi ambaye katika ziara hiyo ameambatana na Kamati ya Usalama ya Mkoa na Kamati ya Wataalamu wamekagua miradi itakayotembelewa na Mbio za Mwenge wa Uhuru katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime kwa mwaka 2025.  

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa