• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC atoa siku 14 Halmashauri kuwasilisha mpango wa ukarabati wa shule kongwe

Posted on: December 12th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Evans Alfred Mtambi leo ameongoza kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Mara (RCC) na kuwataka wakurugenzi kuwasilisha taarifa ya hali ya shule kongwe na mkakati wa ukarabati wa shule hizo.

 “Ninataka kujua shule zote kongwe zilizopo katika Halmashauri na hali yake na mikakati ya Halmashauri katika kuzikarabati shule hizo ili kwa ajili ya usalama wa wanafunzi….fedha zipo tuongeze jitihada katika makusanyo” amesema Mhe. Mtambi.  

Aidha, Mhe. Mtambi amewataka viongozi na watendaji wa Serikali kuwahamasisha wananchi kupeleka watoto shule zitakapofungua Januari, 2025 ili kuwawezesha watoto hao kupata elimu itakayowasaidia kuboresha maisha yao.

“Serikali imewekeza sana na hususan kujenga shule nyingi na kuongeza vyumba vya madarasa katika shule za awali na kwa sasa Mkoa hauna mapungufu tena ya vyumba vya madarasa” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kufuatilia fedha za miradi ya maendeleo zilizopokelewa kwenye mamlaka zao ambazo hazijatumika kutekeleza miradi ya maendeleo kama ilivyokusudiwa na Serikali na kupanga mikakati ya kutekeleza miradi hiyo.

Mhe. Mtambi pia amewata Wakuu wa Wilaya na viongozi wengine wa Serikali kuboresha mfumo wa upokeaji malalamiko ya wananchi pamoja na kuwatembelea wananchi katika maeneo yao.  

Akitoa taarifa kwenye kikao hicho, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Bwana Makwasa Bulenga amesema idadi ya vyumba vya madarasa vilivyopo vinatosheleza mahitaji ya madarasa kwa mwaka wa masomo 2025 na kuwahamasisha wazazi kupeleka watoto shule.

Bwana Bulenga amesema Mkoa umeweka makadirio ya kuandikisha watoto 82,679 wa elimu ya awali na mpaka tarehe 22 Novemba, 2024 jumla ya watoto 14,329 ambao ni sawa na asilimia 17.33 ya watoto wote wanaotarajiwa kuandikishwa.

Bwana Bulenga amesema Mkoa umekadiria kuandikisha wanafunzi 74,223 wa darasa la kwanza na hadi kufikia tarehe 22 Novemba, 2024 Mkoa umeandikisha wanafunzi 19,022 ambao ni sawa na asilimia 25.62 ya lengo la Mkoa.  

Bwana Bulenga amesema Mkoa una jumla ya shule za msingi 979 ma Sekondari 316 na una jumla ya wanafunzi wa shule za msingi 635,842 na wanafunzi wa Sekondari 134,560.

Bwana Bulenga amesema katika mtihani wa kumaliza Elimu ya Msingi mwaka 2024 jumla ya wanafunzi 60,261 walifanya mtihani huo na kati yao wanafunzi 47,034 walifaulu na wamechaguliwa kuingia kidato cha kwanza mwaka 2025 wakati wanafunzi 13,227 walifeli.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa