• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC atoa miezi minne kukamilisha ujenzi wa hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Musoma

Posted on: August 6th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Musoma kukamilisha ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Musoma ndani ya miezi miwili ili iweze kutoa huduma kama ilivyokusudiwa.

Mheshimiwa Hapi ametoa maagizo haya leo tarehe 4 Agosti 2021 wakati alipofanya ziara katika halmashauri hiyo kukagua miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.

“Haiwezekani wataalamu mmekaa tu fedha inakuja mpaka inarudi bila kufanyiwa kitu chochote kile, sasa naagiza hadi kufikia mwishoni mwa Desemba 2021 hospitali hii iwe inatumika na hatutakubali tena visingizio,” alisema Mheshimiwa Hapi.

Aidha amemwagiza Mkuu wa Wilaya ya Musoma kuhakikisha ujenzi wa wodi tatu za wagonjwa katika hospitali hiyo ambayo imeletewa fedha miezi sita iliyopita unaanza na unakamilika kwa haraka.

Mheshimiwa Hapi ameitaka SUMA JKT inayojenga mradi wa ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Musoma kufanya kazi usiku na mchana ili kukamilisha kazi hiyo kwa mujibu wa mkataba.

Awali wakitoa taarifa Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wlaya ya Musoma Bwana Frank Magabiro pamoja na Mhandisi wa wilaya Gibai James Maige wameeleza kuwa mradi wa ujenzi wa hospitali hiyo ulianza kutekelezwa mwaka wa fedha 2018/2019.

Hata hivyo mradi huo haukukamilika kwa sababu fedha zake baada ya muda wa matumizi kuisha zilirudishwa serikalini, baadaye zikaletwa tena Mei, 2021 lakini hadi tarehe 30 Juni 2021 fedha hizo hazikutumika zikarudi tena serikalini.

Aidha walieleza kuwa kwa sasa fedha hizo zimeletwa tena na wapo katika mchakato wa kununua vifaa na kuleta maji eneo la ujenzi ili kukamilisha ujenzi huo.

Wakati huo huo hospitali hiyo ilipokea fedha za ujenzi wa wodi tatu za wagonjwa lakini halmashauri imenunua baadhi ya vifaa vya ujenzi na kufyatua matofali lakini ujenzi haujaanza.

Katika ziara hiyo Mheshimiwa Hapi pia alitembelea mradi wa ujenzi wa ofisi ya Halmashauri ya wilaya ya Musoma, miradi ya Shule ya Sekondari ya Msihakamano, Sekondari ya Ufundi ya Musoma na Bandari ya Musoma inayomilikiwa na Mamlaka ya Bandari Tanzania.

Katika ziara hiyo Mheshimiwa Hapi aliambatana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Albert Gabriel Msovela, Mkuu wa Wilaya ya Musoma Dkt. Alfany Haule, mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Musoma na viongozi wengine.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa