• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC ataka wananchi kulinda miradi ya maji

Posted on: July 16th, 2021

HAPI ATAKA WANANCHI KULINDA MIRADI YA MAJI

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhehsimiwa Ally Salum Hapi amewataka wananchi wa Mkoa wa Mara kulinda miundombinu na vyanzo vya maji ili miradi ya maji inayoletwa na serikali katika maeneo yao iweze kuleta manufaa yaliyokusudiwa.

Hayo yameelezwa katika ziara yake aliyoifanya katika Mji wa Shirati katika Halmashauri ya Wilaya ya Rorya kukagua mradi wa Maji unaosimamiwa na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Musoma (MUWASA).

“Mradi ya maji kama hii inaletwa kwa lengo la kutatua tatizo kubwa la maji ambalo lilikuwepo na linawaathiri kwa kiasi kikubwa wanawake wanaotumia muda mwingi kutafuta maji” alisema Mheshimiwa Hapi.

Amewatahadharisha wanaohujumu miundombinu ya maji kuwa serikali haitawafumbia macho kuona wananchi wengi wanataabika kwa sababu ya watu wachache wanaohujumu kwa manufaa yao.

Mkuu wa Mkoa amemuagiza Kamanda wa Polisi wa Wilaya ya Kipolisi Shirati kuwatafuta watu waliohujumu bomba la mradi wa maji Shirati tarehe 11 Julai 2021 na kusababisha hasara kwa serikali na wananchi wa Mji wa Shirati kukosa huduma ya maji.

Wakati huo huo, Mheshimiwa Hapi alitoa ofa kwa wananchi wa Mji wa Shirati kuunganishiwa huduma ya maji majumbani kwa mkopo baada ya kulipia nusu ya gharama inayohitajika kuunganisha maji.

“Ninatoa ofa kuanzia sasa mtu yeyote atakayehitaji kuunganishiwa maji anaweza kujiandikisha na kulipa nusu ya gharama ya kuunganishiwa maji na ataunganishiwa maji kwa mkopo kuanzia tarehe 01 Agosti 2021” alisema Mheshimiwa Hapi.

Amewahamasisha wanaume kuchukua fursa hiyo kuunganisha maji kwa ajili ya familia zao ili kuwaacha wanawake waendelee kufanya shughuli nyingine za kiuchumi.

Awali, akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi wa ukarabati wa miundombinu ya maji wa Shirati, Mkurugenzi wa MUWASA CPA Joyce Msiru ameeleza kuwa watu wasiojulikana walikata bomba la mradi huo lenye ukubwa wa nchi tisa na kusababisha shida ya maji kwa wakazi wa Mji wa Shirati.

Hata hivyo Bibi Msiru ameeleza kuwa kwa sasa bomba hilo limetengenezwa na upatikanaji wa maji umerejea katika hali yake ya kawaida baada ya bomba lililokatwa kutengenezwa.

“Kwa sasa huduma ya maji inapatikana kwa asilimia 20 ya wakazi wote wa Mji wa Shirati na mpaka sasa jumla ya wateja 494 wameshaunganishiwa maji majumbani na wengine waliobakia wanachota maji kwenye vioski vya maji” alisema CPA Msiru.

Bibi Msiru ameeleza kuwa MUWASA imepewa jukumu la kusimamia mradi huo kufuatia ziara ya Waziri wa Maji aliyoifanya katika Wilaya ya Rorya Tarehe 6 Januari 2021 baada ya Mji wa Shirati kukosa maji kuanzia mwaka 2015 baada ya kuharibika kwa mradi uliokuwepo.

Ameeleza kuwa baada ya mradi wa ukarabati kukamilika, Wizara ya Maji ilikabidhi mradi huo kwa MUWASA kwa ajili ya kuuendesha kwa muda.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mara Mheshimiwa Samweli Kiboye maarufu kama Namba 3 akizungumza katika mkutano wa wananchi amemuaomba Mkuu wa Mkoa kufuatilia suala la kuanzisha Mamlaka ya Mji Mdogo wa Shirati.

“Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa hapa wananchi hawa kilio chao cha muda mrefu ni kuanzishwa kwa Mamlaka ya Mji Mdogo wa Shirati, wananchi wanatamani sana kuanzishwa kwa mamlaka hiyo” alisema Mheshimiwa Kiboye.

Ameeleza kuwa kwa sasa Mji wa Shirati unawakazi wengi sana wanaojishughulisha na shughuli mbalimbali za kujiingizia kipato.

 Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa aliambatana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Albert Gabriel Msovela; Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mara na Wilaya ya Rorya, wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Rorya, Katibu Tawala wa Wilaya ya Rorya na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya na viongozi wengine.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa