• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC ataka ushirikiano wa viongozi kuleta mabadiliko Mara

Posted on: August 6th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Meja Jenerali Suleiman Mzee leo tarehe 6 Agosti, 2022 amewasili katika Mkoa wa Mara na kuwataka viongozi wa Mkoa huo kushirikiana katika kuleta mabadiliko ya kimaendeleo na kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi wa Mkoa wa Mara.  

Akizungumza baada ya mapokezi yake yaliyofanyika leo baada ya kuwasili, Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa viongozi wa Mkoa wa Mara wakishirikiana vizuri wananchi watapata maendeleo kwa haraka zaidi.  

“Mimi nitajitahidi kuwa mvumilivu maana Mheshimiwa Rais (Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan) alisema huku ni uraiani, lakini sitakuwa mvumilivu na mtu yoyote anayekwamisha au anayechelewesha miradi ya maendeleo ya wananchi wa Mkoa wa Mara” alisema Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee amewaomba viongozi wa Mkoa wa Mara kutoa ushirikiano  katika kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi.  

“Hapa tupo kwenye ziwa, kilimo chetu bado kinategemea mvua, lakini tukishirikiana tutatafuta ufumbuzi wa kuweza kutumia maji ya ziwa katika kilimo cha umwagiliaji na kuwasaidia zaidi wakulima” alisema Mheshimiwa Mzee.  

Aidha, Mheshimiwa Mzee amewataka viongozi kushiriki kikamilifu katika maandalizi na uhamasishaji wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 ili Mkoa wa Mara uweze kufanya vizuri katika zoezi hilo kwa manufaa ya wananchi na Taifa kwa ujumla.  

“Mimi ninawaomba tushirikiane vizuri katika maandalizi na hususan uhamasishaji wa wananchi katika kushiriki kikamilifu katika zoezi la Sensa ili Sensa ya mwaka huu ifanyike vizuri katika Mkoa wetu” alisema Mheshimiwa Mzee.

Mkuu wa Mkoa amepokelewa na viongozi wa Mkoa wa Mara wakiongozwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu katika eneo la Ndabaka, Wilaya ya Bunda ambapo ni mpakani kati ya Mkoa wa Mara na Mkoa wa Simiyu katika Barabara ya Mwanza- Musoma- Sirari.

Baada ya mapokezi hayo, viongozi hao walielekea ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara ambapo Mkuu wa Mkoa alisaini kitabu na kuzungumza na viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Mara walioshiriki mapokezi hayo.

Viongozi wengine waliokuwepo katika mapokezi hayo ni Wakuu wa Wilaya, Kamati ya Usalama ya Mkoa, baadhi ya viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mara, Wakuu wa Idara na Vitengo vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Makatibu Tawala wa Wilaya na baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Meja Jenerali Suleiman Mzee ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara tarehe 31 Agosti, 2022 kuchukua nafasi ya Mheshimiwa Dkt. Raphael Chegeni aliyeteuliwa tarehe 28 Agosti, 2022 kuchukua nafasi ya Mheshimiwa Ally Salum Hapi ambaye uteuzi wake umetenguliwa.  

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa