• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC Ataka JKT Rwamkoma kuboresha huduma Butiama

Posted on: September 23rd, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee amekitaka Kikosi cha Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) 822 Rwamkoma kusaidia katika kuboresha upatikanaji wa huduma za kijamii katika Wilaya ya Butiama.

Mheshimiwa Mzee ametoa rai hiyo wakati alipokitembelea kikosi hicho kwa ajili ya kufunga mafunzo ya vijana 891 waliopata mafunzo kwa mujibu wa sheria katika operesheni ya Jenerali Venance Mabeyo, 2022.

“Katika Wilaya ya Butiama hamna sehemu nzuri ya watu kupumzika na kupata huduma za chakula na vinywaji kwa hadhi ya wageni wa kitaifa na kimataifa wanayoitembelea Butiama, hivyo mkiboresha huduma watu na hususan wageni watakuja” alisema Mheshimiwa Mzee.

Aidha, Mheshimiwa Mzee amekitaka kikosi hicho kuongeza biashara zake inazozifanya katika eneo hilo na kufungua kiwanda cha kutengeneza mikate, duka la mboga mboga pamoja na kufungua duka katika Mji wa Musoma ili kuuza bidhaa mbalimbali wanazozalisha.

Akiwa katika eneo hilo Mheshimiwa Mzee amefungua Bwalo la Maafisa wa Jeshi na kupanda mti wa kumbukumbu, ametembelea mashine ya kuzalisha chakula cha Samaki, kukagua gwaride la vijana na kutoa zawadi kwa vijana waliofanya vizuri katika mafunzo hayo.

Akitoa taarifa kwa Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Kikosi hicho Luteni Kanali Gaudensia Joseph Mapunda ameeleza kuwa mafunzo ya vijana hao yameanza tangu tarehe 27 Juni, 2022 na kuhusisha vijana 904 hata hivyo 13 hawakumaliza mafunzo kutokana na utoro.

“Kati ya vijana waliopangiwa kufanya mafunzo yao katika kikosi hicho, vijana 206 walikuwa ni wasichana huku 698 walikuwa ni wavulana”alisema Bibi Mapunda.

Luteni Kanali Mapunda ameeleza kuwa vijana hao waliohitimu mafunzo yao wamefanya mafunzo mbalimbali kwa nadharia na kwa vitendo na sasa wapo tayari kulitumikia Taifa.

Aidha, Bibi Mapunda alisema kuwa Bwalo la Maafisa wa Jeshi lililofunguliwa limegharimu zaidi ya shilingi milioni 53 na ujenzi wake umekamilika.

Ameitaja miradi mingine inayoendeshwa na kikosi hicho kuwa ni pamoja na kilimo, ufugaji wa ng’ombe na Samaki, bucha, ufugaji wa nyuki na biashara ya chakula na vinywaji katika eneo la Rwamkoma na Viwanja vya Nyakabindi, Simiyu.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Butiama, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mara na Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Butiama.  

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa