• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC apongeza Wilaya ya Musoma uandikishaji wanafunzi

Posted on: January 18th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda leo amezungumza na Waandishi wa Habari ofisini kwake na kutoa taarifa ya uandikishaji na mapokezi ya wanafunzi wa Darasa la Awali, Darasa la Kwanza na Kidato cha Kwanza hadi kufikia tarehe 17 Januari, 2024 na ameipongeza Wilaya ya Musoma kwa kufanya vizuri katika uandikishaji.

MHe. Mtanda ameeleza kuwa taarifa zinaonyesha kuwa Wilaya ya Musoma kupitia Halmashauri zake za Halmashauri ya Wilaya ya Musoma na Manispaa ya Musoma zimefanya vizuri katika uandikishaji na mapokezi ya wanafunzi.

“Ninaipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Musoma kwa kuongoza kimkoa katika kuandikisha wanafunzi wa Darasa la Awali na kidato cha Kwanza na Manispaa ya Musoma kwa kuongoza katika kuandikisha wanafunzi wa darasa la Kwanza” amesema Mhe. Mtanda

Mkuu wa Mkoa amewataka viongozi wa Wilaya, Halmashauri, Watendaji wa Kata na Vijiji kuhakikisha wanafunzi wote waliotarajiwa kuanza masomo kwa mwaka 2024 wanapelekwa shule na wanaanza masomo.

“Nitoe wito kwa Wakuu wa Wilaya na viongozi wa ngazi zote kuhakikisha wanafanya msako wa wanafunzi wote wanaotakiwa kwenda shule wanaanza masomo kabla ya mwisho wa muda wa kupokea wanafunzi kwa mwaka 2024” amesema Mhe. Mtanda.

Mhe. Mtanda amewapongeza viongozi wote, wasimamizi wa Elimu, walimu wakuu na wakuu wa shule kwa kazi kubwa wanayoifanya na kuwataka kuhakikisha kuwa wanafunzi wote wanaotakiwa kuanza masomo wanaanza masomo bila vipingamizi.  

Taarifa iliyotolewa na Kaimu Katibu Tawala Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Bwana Bulenga Makwasa imeeleza kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma imeandikisha jumla ya wanafunzi 9,212 ambapo kati yao wavulana ni 4692 na wavulana ni 4520 sawa na asilimia 96.56 ya watoto 9,540 waliotarajiwa kuandikishwa Darasa la Awali.

Halmashauri nyingine zilizofanya vizuri uandikishaji wa Darasa la Awali ni pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti iliyoandikisha kwa asilimia 95.81 na Halmashauri ya Wilaya ya Butiama  iliyoandikisha kwa asilimia 91.99.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Halmashauri ya Wilaya ya Musoma pia imefanya vizuri katika uandikishaji wa wanafunzi wa Kidato cha Kwanza ambapo imeandikisha wanafunzi 4,092 kati ya wanafunzi 5733 waliofaulu na kuchaguliwa kujiunga na Shule za Sekondari katika Halmashauri hiyo ambayo ni sawa na asilimia 71.

 Halmashauri nyingine zilizofanya vuzuri uandikishaji wa Kidato cha Kwanza ni Manispaa ya Musoma asilimia 69.36, Halmashauri ya Mji wa Bunda asilimia 62.13.

Aidha, taarifa hiyo imeonyesha kuwa Manispaa ya Musoma imefanikiwa kuandikisha wanafunzi 4,482 Darasa la Kwanza kati ya maoteo ya kuandikisha wanafunzi 4,437 kwa mwaka 2024 ambayo ni sawa na asilimia 101.01.   

Halmashauri nyingine zilizofanya vizuri katika uandikishaji wa Darasa la Kwanza ni Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti asilimia 99.81, Halmashauri ya Wilaya ya Rorya asilimia 96.18.

 Uandikishaji wa wanafunzi unaendelea hadi tarehe 31 March, 2024 ambapo utasitishwa hadi mwaka uandikishaji kwa ajili ya mwaka mwingine wa masomo utakapoanza.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa