• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC apokea maafisa wa Israel

Posted on: August 25th, 2022

RC APOKEA MAAFISA WA ISRAEL

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mzee leo tarehe 24 Agosti, 2022 amewapokea maafisa wanne kutoka Tel Aviv Sourasky Medical Center, Lis Maternity and Women’s Hospital kutoka nchini Israel ambao wamekuja kwa ajili ya kuanzisha mradi mpya wenye lengo la kuboresha huduma za afya ya uzazi katika Mkoa wa Mara.

Akizungumza baada ya kuwapokea maafisa hao, Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa amefurahi sana kwa nchi ya Israel kuanzisha mradi wa kuimarisha huduma za afya kwa wananchi wa Mkoa wa Mara na kuwaahidi wataalamu hao kuwa Mkoa wa Mara utawapa ushirikiano katika kutelekeza mradi huo.  

Katika Mapokezi hayo, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu, wataalamu wa afya na baadhi ya maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Maafisa waliopokelewa kutoka Israel ni Dkt. Gilard Rattan Moshe, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Akina Mama, Binat Sessan, Muuguzi Mkunga na Mkuu wa Wodi ya Wazazi, Rinat Segal, Muuguzi Mkunga na Mkuu wa Mafunzo na Revital Levi Ari, Muuguzi Mkunga na Mkuu wa Kitengo cha Tiba Mbadala wa hospitali ya Tel Aviv.  

Aidha, maafisa hao wamewasilisha nyaraka za msaada wa vifaa tiba mbalimbali vyenye thamani ya zaidi ya Dola za Kimarekani 13,500 ambayo Serikali ya Israeli imetoa kwa ajili ya vituo vya kutolea huduma za afya katika Mkoa wa Mara.

Wakizungumza wakati wa kupokea taarifa ya sekta ya afya ya Mkoa wa Mara, maafisa hao kutoka Israel wameahidi kuendelea kutoa msaada wa vifaa tiba na mafunzo ya muda mfupi kwa madaktari wa kawaida ili waweze kufanya vizuri operesheni za uzazi katika maeneo yao.

“Katika nchi nyingi zilizoendelea madaktari wa kawaida hawaruhusiwi kuwafanyia operesheni kwa akina mama wajawazito, lakini huku kutokana na upungufu wa madaktari bingwa, madaktari wa kawaida ambao hawana utaalamu na masuala ya uzazi wanaruhusiwa kuwafanyia upasuaji wajawazito jambo ambalo linaweza kuwa ni hatari” walisema wataalamu hao.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Afya Dkt. Juma Mfanga amewashukuru wageni hao kwa kutaka kuanzisha mradi katika Mkoa wa Mara na kuwasilisha nyaraka za msaada huo na kuwaahidi Mkoa wa Mara utawapa ushirikiano wa kutosha katika kuimarisha ushirikiano baina ya Israeli na Tanzania.

Mbali na kuembelea Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, wataalamu hao pia wametembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara katika eneo la Kwangwa na vituo mbalimbali vya kutolea huduma za afya katika Mkoa wa Mara.

Kabla ya kuja Mkoa wa Mara, wataalamu hao walikutana na Mganga Mkuu wa Serikali kutoka Wizara ya Afya, Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Afya na Mkurugenzi wa Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe kutoka Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).  

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa